21/07/2026
Tabora, wakati umefika!
Kesho, tarehe 22 Julai 2026, Puma Energy Tanzania itazindua rasmi kituo chake cha kwanza Mkoani Tabora, ambacho pia ni kituo cha 100 nchini. Hii ni hatua muhimu katika safari yetu ya kuendelea kuwafikishia Watanzania huduma bora za nishati.
Uzinduzi huo utahudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Paulo Matiko Chacha, ambaye atakuwa mgeni rasmi. Kituo kinapatikana roundabout ya kuelekea Ikulu, Tabora.
Kupitia kituo hiki, wakazi wa Tabora watapata huduma za mafuta ya ubora, Puma Lubricants, PumaGas pamoja na fursa ya kukusanya points za Puma Pris kila wanapotumia huduma zetu.
Karibu tuadhimishe pamoja uzinduzi wa kituo chetu cha kwanza Tabora na mafanikio ya kufikisha vituo 100 nchini Tanzania.