BFR Builders

BFR Builders BFR Builders tupo mkoa wa Dar es Salaam. Tunajihusisha na shughuli zifuatazo.
1. House design ( Arc

JIPATIE RAMANI ZA NYUMBA KWA BEI NAFUUNyumba hii 👇👇👇1. Ina Vyumba Vinne(4), Kimojawapo ni Master2. Ina Sebure kubwa na D...
30/08/2020

JIPATIE RAMANI ZA NYUMBA KWA BEI NAFUU
Nyumba hii 👇👇👇
1. Ina Vyumba Vinne(4), Kimojawapo ni Master
2. Ina Sebure kubwa na Dinning room
3. Ina Jiko + Store + Public Toilet..
: 👉 0686054161
Ushauri wa Kitaalamu Tunatoa BURE

Nyumba ya vyumba vitatuâ—Ź 1 Master bedroomâ—Ź 1 Self Contained roomâ—Ź 1 Plain bedroomâ—Ź Sitting room, Dining, Kitchen & Store...
23/08/2020

Nyumba ya vyumba vitatu
â—Ź 1 Master bedroom
â—Ź 1 Self Contained room
â—Ź 1 Plain bedroom
â—Ź Sitting room, Dining, Kitchen & Store
â—Ź Public toilet

Mahitaji

â—Ź Tofali za msingi = 1250 ( inch 6)
â—Ź Tofali za boma = 2400 ( inch 5)
â—Ź Mifuko ya Cement kwaajili ya kujengea = 105
â—Ź Nondo = pcs 65 ( size 12mm) kwaajili ya mkanda, nguzo na lintel
â—Ź Trip 3 ( @ 4 cubic metres) za mchanga kwaajili ya msingi
â—Ź Trip 2 ( @ 4 cubic metres) za kokoto kwaajili ya mkanda na lintel
â—Ź Bati = pcs 80 ( zenye urefu wa futi 10)
â—Ź Mbao = 2x4 (pcs 130), 2x2 ( pcs 110)

Eneo la nyumba : 14m x 10m ( sqm 140)

Tuwasiliane : 0719297390

Kutana na wataalamu wa Urembo wa nguzo, madilisha mkanda hachi,Namba 0716070965/ 0744207399
11/08/2020

Kutana na wataalamu wa Urembo wa nguzo, madilisha mkanda hachi,
Namba 0716070965/ 0744207399

26/07/2020

High quality and reliable services

Design & Construction supervision. ..Preparation of BOQ & Cost estimation. .Tuone kwa huduma bora na ya kuaminika.
13/07/2020

Design & Construction supervision. ..
Preparation of BOQ & Cost estimation.
.
Tuone kwa huduma bora na ya kuaminika.

  (Fuata sheria, Epuka Usumbufu)  Tupigie 0656558445 / 0686054161   Kulingana na sheria ya ujenzi wa majengo Mijini si r...
30/09/2019


(Fuata sheria, Epuka Usumbufu)


Tupigie 0656558445 / 0686054161

Kulingana na sheria ya ujenzi wa majengo Mijini si ruhusa kwa mtu yeyote kujenga au kuanza kujenga jengo bila ya:-
(i) Kutuma maombi kwa mamlaka ya mji
(ii) Kuwasilisha michoro ya jengo na kumbukumbu husika
(iii) Kupata kibali kwa maandishi kinachoitwa “Kibali Cha ujenzi”

2. KIBALI CHA AWALI (Planning consent)
Inashauriwa kupata kibali cha awali kabla ya kuomba kibali cha ujenzi. Hivyo muendelezaji anatakiwa aandae mchoro wa awali (Outland plan) kwa utaratibu unaotakiwa ukionyesha aina ya ujenzi atakaokusudia kufanya ili aweze kupata ridhaa ya kuendelea na hatua za kuandaa michoro ya mwisho.
Faida:
• Kuokoa muda na gharama iwapo michoro ya mwisho itaonekana kuwa na dosari za kitaalam ambazo zitahitaji kufanyiwa marekebisho.
•Kuwa na uhakika kuhusu mahitaji muhimu ya kuzingatiwa wakati michoro inaandaliwa.

3. JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI YA KIBALI CHA UJENZI
Baada ya michoro kukamilika, iwasilishwe ikiwa kwenye majalada kwa namna ambayo inaweza kufunguliwa na kusomeka. Michoro hiyo iwasilishwe ifuatavyo:-
• Seti tatu za michoro ya jengo (Archectural drawing)
• Seti mbili za michoro ya vyuma/mihimili (structural drawings) kwa michoro ya ghorofa

4. MICHORO ILIYOANDALIWA IONYESHE NINI
Michoro itakayoandaliwa inatakiwa ionyeshe mambo yafuatayo:-
• Namna jengo litakavyokuwa (plans, sections, elevations, foundation and roof plan)
• Namba na eneo la kiwanja kilipo
• Jina la mmilikaji ardhi inayohusika
• Jina la mchoraji, ujuzi na anwani
• Ukubwa wa jengo kwa mita za mraba
• Ujazo wa kiwanja (Plot coverage)
• Uwiano (Plot ratio)
• Matumizi yanayokusudiwa
• Idadi ya maegesho yatakayokuwepo
• Umbali wa jengo kutoka kwenye mipaka ya kiwanja (setbacks)
• Mfumo wa kutoa maji taka hadi kwenye mashimo

5. VIAMBATANISHO
• Fomu za maombi zilizojazwa kwa usahihi
• Hati ya mmiliki wa kiwanja au barua ya toleo
• Kumbumbuku nyingine zinazohusu kiwanja hicho k**a hati za mauzo, makabidhiano n.k
• Nakala za risiti ya kodi ya kiwanja na kodi ya majengo
• Mabadiliko ya matumizi ya ardhi

6. HATUA ZINAZOFUATWA KATIKA KUSHUGHULIKIA MAOMBI YA KIBALI
Zifuatazo ni hatua zinazofuatwa wakati wa kuchunguza michoro hiyo:-
• Uhakiki wa miliki
• Kukaguliwa usanifu wa michoro
• Kukagua kiwanja kinachokusudiwa kuendelezwa
• Uchunguzi wa matumizi ya jengo na uwiano
• Uchunguzi wa maofisa wa afya
• Uchunguzi wa mipango ya uondoaji maji taka
• Uchunguzi wa tahadhali za moto
• Uchunguzi wa uimara wa jingo
• Kuwasilishwa kwenye kikao cha Mipangomiji na Mazingira baada ya kukamilisha taratibu zote
• Hatimaye kuandika na kutoa kibali

7. TARATIBU ZA KUFUATA BAADA YA KUPATA KIBALI CHA UJENZI

Kwa mujibu wa sheria ya ujenzi mijini ujenzi wowote ambao
umepata kibali unapaswa kukaguliwa kwa kila hatua ya ujenzi. Baada ya kupata kibali cha ujenzi mambo yafuatayo yanapaswa kufanyika:-

1. Kutoa notisi ya masaa 48 kabla ya kuanza ujenzi.
Fomu ya notisi hii utapatiwa unapokabidhiwa kibali cha ujenzi

2. Kujaza fomu ya ukaguzi na kuwasilisha kwenye ofisi ya ujenzi ili hatua hiyo ya ujenzi unayotaka kufanya ikaguliwe

3. Utapatiwa “Certificate of Occupation” baada ya ujenzi wako kukamilika iwapo tu hatua muhimu za ujenzi zimekaguliwa

8. FAIDA ZA KUJENGA NYUMBA IKIWA NA KIBALI CHA UJENZI

1. Kuishi kwenye nyumba ambayo imethibitishwa kitaalamu kuwa ni salama

2. Kuwa na mazingira bora kwa kuwa na mji uliopangwa

3. Kuepuka hasara na usumbufu unaoweza kutokea iwapo ujenzi umefanyika bila kibali ikiwa pamoja na kush*takiwa mahak**ani, kuvunjiwa na kulipa gharama za uvunjaji.

Hayo ndio Mambo muhimu ya kuyafahamu kuhusu 'Kibali cha Ujenzi' (Building Permit), Epuka usumbufu fuata sheria!


Tupigie 0656558445 / 0686054161

 Watu wengi wanakumbwa na jaribu kali sana la kukimbilia moja kwa moja kwenye kuanza ujenzi. Je mara tu unapoanza utafan...
30/09/2019



Watu wengi wanakumbwa na jaribu kali sana la kukimbilia moja kwa moja kwenye kuanza ujenzi. Je mara tu unapoanza utafanya sawa? Kwa bahati mbaya wengi hukwama kuendelea na ujenzi ikiwa haujafanya mipango muhimu kabla. Kila mtaalamu wa Kudesign na Fundi ujenzi hata Engineer anaendesha biashara yake kwa njia tofauti, Lakini wamiliki wa nyumba kawaida wanahitaji kufuata hatua sawa ili kufikia awamu ya ujenzi.
Ukiwa na kiwanja chako safi Fuata hatua sita muhimu za kukusaidia kupanga ujenzi wa nyumba ili kufikia lengo lako bila kukwama njiani, Na ni muhimu sana kwa mradi wowote wa ujenzi.

#1.Chagua Mtaalamu au Msanifu (Designer)

Kuchagua msanifu wa muundo kawaida huanza kukutana na mhusika mwenyewe, ambayo inaweza kuchukua wiki chache kulingana na kampuni au wataalamu wangapi unahoji. Hii ni nafasi yako ya kuelewa huduma ambazo kila kampuni hutoa na hakikisha zinaendana na kile unachotarajia. Ni muhimu pia kuwa na bajeti ya mradi wako akilini kwamba unawasiliana wazi na kampuni unayoajiri, kwa hivyo muundo unaweza kuendana na kile unachopanga kuwekeza.

#2.Unda au Sanifu Jengo lako
Baada ya kuchagua kampuni au mtaalamu, ni wakati wa kuanza kazi. Kawaida kuna angalau walau mbili na wakati mwingine njia tatu nzuri za kufikia malengo yako ya kusanifu jengo.
Kawaida lazima kuwe na muundo wa awali, huu utaonesha ramani ya nyumba na hata muonekano wa nje baada ya ujenzi. Kupitia muundo wa awali na kwa kushauliana na mtaalamu yawezekana yakafanyika mabadiliko kwa kuongeza vitu au kupunguza vitu mpaka kufikia kusudi lako. Hii itasaidia pia kuweza kuwa na makadilio ya awali ya gharama za ujenzi
#3.Tafuta Mkandarasi au Fundi ujenzi

Tafuta na kuhoji wakandarasi mbalimbali au mafundi ujenzi mbalimbali kuhusiana na mradi au aina ya jengo unalokusudia kulijenga. Jinsi unavyowahoji utaweza kupata makadilio ya gharama utakazotakiwa kulipia kwa ajili ya mkandarasi au fundi pia utaweza kupata ushauri wa ziada kuhusiana na mradi wako kutegemeana na uzoefu wa fundi au mkandarasi.
Hakikisha muda wa kuchagua mkandarasi au fundi unazingatia vigezo vikuu viwili; Uzoefu wake kwenye ujenzi na Unafuu wa gharama anayokutajia, Ila ya kwanza ni muhimu zaidi maana suala la gharama mnaweza kuelewana

#4.Fanya Window Shopping

Fanya utafiti na upate gharama za vifaa vyote utakavyohitaji kwa ajili ya ujenzi wako, hii inahusisha Vinapatikana wapi? Vipo umbali gani? Vinauzwaje? Na je vipo kwa kiasi cha kutosha?
Haya ni maswali muhimu ili kuweza kukadilia ni kiasi gani vifaa vya ujenzi vitakugharimu

#5.Tafuta kibari cha ujenzi

Kulingana na ukubwa wa mradi wako au aina ya mradi wako na sehemu ulipo, idhini inaweza kuchukua siku, miezi au hata miaka. Unapaswa kuwa na wazo fulani kabla ya kutafuta vibali kuhusu urefu wa mchakato, ambayo itakuruhusu kutambua tarehe inayoweza kuanza ya mradi wako. Haya yote yanategemeana kulingana na wapi unaishi na jinsi mradi wako ni mkubwa.

#6.Sasa uko tayari kuanza

Pamoja na mpango uliyowasilishwa kwa vibali na chaguzi za nyenzo zilizofanywa, kontrakta wako ataweza kumaliza kuweka bei na kuandika mkataba wa ujenzi. Ikiwa vifaa vilivyochaguliwa vinagharimu zaidi ya bajeti inavyoruhusu, kunaweza kuwa na duru ya "uhandisi wa thamani," ambayo inamaanisha kubadilisha wigo wa kazi au vifaa ili kupunguza gharama. Kufikia wakati mkataba unasainiwa, kontrakta wako atakuwa amegundua vitu vinavyoongoza kwa muda mrefu (k**a makabati, windows, milango, tiles na wakati mwingine bomba au vifaa vya umeme) na anaweza kuwa nayo kwa mpangilio kabla ya kuanza kwa ujenzi, kulingana na muda wa mradi wako.
Kufikia wakati hatua zote hizi zimekamilika, inaweza kuwa miezi nne hadi sita au zaidi tangu ulianza kuzungumza na wataalamu wa kubuni au hata pungufu ya muda huo kutegemeana na uwezo wako kifedha
Mchakato wa kupanga unaweza kuwa mrefu, lakini kila hatua unayochukua itakuweka karibu na kuanza mradi wako na maono dhahiri ya kitakachokuja. Uwekezaji wa wakati kwenye mradi wakoe unamaanisha timu yako yote ya ujenzi - mtaalamu wa kubuni au designer, mkandarasi na wewe -, " Sasa Nenda!" Bila kusita.

  Pata ramani ya Nyumba ya ndoto zako kwa garama nafuu.Huduma Tunazotoa ni pamoja na:1. Kudesign Nyumba kulingana na Mah...
18/09/2019


Pata ramani ya Nyumba ya ndoto zako kwa garama nafuu.
Huduma Tunazotoa ni pamoja na:
1. Kudesign Nyumba kulingana na Mahitaji yako
2. Kujenga Nyumba kwa garama nafuu
3. Kufanya Landscaping na Gardening
4. Kudesign na kujenga Maegesho ya magari ( Parking design)

Tupigie 0656558445 / 0686054161.

Kutana na wataalamu, kwa kazi za uhakika na kwa kiwango cha hali ya juu.. Piga  0656558445LandscapingParking design & Ga...
16/09/2019

Kutana na wataalamu, kwa kazi za uhakika na kwa kiwango cha hali ya juu.. Piga 0656558445
Landscaping
Parking design &
Gardening.

Address

Kinondoni
Dar Es Salaam

Telephone

+255686054161

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BFR Builders posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to BFR Builders:

Share