13/04/2026
Mpendwa Mzazi,
Pokea Salamu kutoka Tanzania Technology Community (TTC).
Tunayo furaha kumualika mtoto wako kushiriki katika:
Student Innovation & Digital Exhibition 2026
Yenye Kauli mbiu: _From Classroom to Real-World Impact._
Hii ni fursa ya kipekee inayolenga kuwasaidia wanafunzi kubadilisha yale wanayojifunza darasani kuwa miradi halisi na ubunifu wa vitendo.
Faida kwa mtoto wako:
✅ Kujiamini katika kuwasilisha mawazo
✅ Ujuzi wa kidijitali wa vitendo (Teknolojia, Ubunifu & Uvumbuzi)
✅ Uwezo wa kutatua matatizo na kufikiri kwa kina
✅ Uzoefu wa kutumia masomo ya darasani katika maisha halisi
✅ Mwongozo (mentorship) kutoka kwa wataalamu wenye uzoefu
Jinsi inavyofanyika:
Mwezi Aprili na Mei
Wanafunzi wataongozwa hatua kwa hatua kuunda miradi rahisi au ya kiwango cha juu
Hata k**a mtoto wako hana wazo bado, tutamsaidia kuligundua na kulijenga
Wanafunzi wenye miradi tayari wanakaribishwa kujisajili kwa ajili ya ukaguzi na kuionesha moja kwa moja siku ya tukio.
Mifano ya miradi:
1. Kutengeneza programu au mchezo rahisi wa kompyuta
2. Kubuni uwasilishaji wa kidijitali au kitabu
3. Kutatua changamoto ya jamii kwa kutumia teknolojia
4. Miradi ya sayansi au ubunifu
5. Miradi ya roboti (Robotics)
6. Miradi ya coding n.k
Kwa nini hii ni muhimu:
Katika dunia ya leo, mafanikio hayategemei tu kufaulu mitihani, bali uwezo wa mtoto kuunda, kutatua matatizo, na kuwasilisha mawazo yake.
Programu hii itamsaidia mtoto wako kutoka:
👉 Kujifunza darasani tu
➡️ kwenda
👉 Kutumia maarifa katika maisha halisi
Tunakukaribisha kwa moyo mkunjufu mtoto wako awe sehemu ya safari hii ya mabadiliko.
📞 Usajili & Mawasiliamo zaidi:
Call / WhatsApp:
📱 +255 715 334 256
📱 +255 779 240 375
Tujenge pamoja kizazi cha wabunifu. 🌍✨
Imetolewa na,
Tanzania Technology Community (TTC)
Innovation | Technology | Education