27/05/2026
KWANINI GHARAMA ZAKO ZA MATUMIZI YA UMEME ZIKO JUU SANA?
Watu wengi wanalipa bili kubwa za umeme tofauti na mategemeo yao. Hizi hapa sababu za gharama kubwa ya umeme.
1. Utofauti wa Bei za Umeme kutoka TANESCO
Mtu mmoja aliuliza Kwa nini wengine wakitoa Tshs 10,000/= wanapata umeme mwingi kuliko mimi? Jibu ni kwamba Bei ya umeme inatofautiana kutokana na kundi la matumizi ulilopo. Kwa mfano Mtu mwenye matumizi Madogo ya nyumbani mita yake ya LUKU itakuwa imesajiliwa na TANESCO kwenye Tarrif D1. Hivyo kutofautiana kwa kundi la matumizi ndicho kinachopelekea watu kupata unit tofauti kwa kiasi kilekile cha pesa., na hapa wengine hudhani wanatumia zaidi
2. Matumizi yasiyo sahihi ya vifaa umeme
Kuna watu wanaolipa bili kubwa ya umeme kwa sababu wanatumia vibaya Vifaa vya umeme. Mifano halisi ni hii. Kuwasha kiyoyozi (AC) alafu umefungua milango na madirisha, umeme unatumika bure na hupati baridi ndani. Kuacha vifaa vingi vikiwa vimechomekwa kwenye soketi muda mrefu. Kwa mfano unapoacha pasi ya umeme au wimbi mikro (Microwave) au TV usiku kucha au au hata chaja ya simu ikiwa imechomekwa kwenye soketi.
3. Kutumia vifaa vinavyotumia umeme mwingi
Kuna Vifaa ambavyo hutumia umeme mwingi sana. Kwa mfano kuna taa ya umeme ya Wati 10 inatoa mwanga mkali kuliko taa ya wati 30. Hii ambayo ni kubwa na mwanga mdogo ni kwa sababu inapoteza umeme mwingi ambao wewe unaulipia.
4. Kutumia vifaa vya umeme ambavyo ni vibovu vina tabia ya kunyonya umeme mwingi kuliko kawaida.
5. Umeme Kutoka TANESCO ukiwa na hitilafu
6. Uchakabu wa mfumo wa umeme kwenye jengo. Wayaring ikishakaa miaka 30 au zaidi inahitaji kubadilishwa au kuboreshwa sana.
7. Makosa ya kiufundi kwenye mfumo, k**a kuunganisha kimakosa live na earth, au kutoweka RCD kwenye main switch, au kuwepo kwa resistance kubwa kwenye saketi ya earth,
Mambo ni mengi. Kwa msaada wa kitaalam, wasiliana na VOX ENGINEERING KWA NUMBER 0714136897
KARIBU TUKUHUDUMIE.
VOX, Kasi ya Kazi