Mwalimu Bora Daima

Mwalimu Bora Daima 🔴 Educational & Awareness
🔴 Agribusiness
🔴 Industrial, Trade, Investment & Commercial
🔴 Services

07/01/2025
01/11/2024

: Kanuni za Afya

:

⚠️ Usile chakula cha moto (kunywa maji ya moto) kwenye chombo cha plastiki.
Plastiki ikichemka huzalisha mlundikano wa kemikali inayosababisha aina 52 za Saratani

⚠️ Tumia Sikio la Kushoto unapozungumza kupitia simu ya mkononi 📵

⚠️ Usimeze dawa kwa kutumia maji ya baridi

⚠️ Usile chakula kizito au kinachotia nguvu mwilini baada ya saa 11 jioni

⚠️ Kunywa maji mengi wakati wa asubuhi na maji kidogo wakati wa jioni

⚠️ Epuka kunywa kimiminika wakati wa kula au muda mfupi baada ya kula kwa mmeng’enyo bora.
Matumizi ya kimiminika k.v. maji, chai, soda, n.k wakati au muda mfupi baada ya kula ni chanzo cha maumivu ya tumbo, tumbo kujaa gesi, kupungua kwa nguvu ya tindikali, nk

⚠️ Usilale muda mfupi baada ya kula

⚠️ Funga

▶️ Kwaresma
🔘Wayahudi Wacha Mungu (Jumatatu na Alhamisi)
🔘Himaya ya Kirumi; kufunga k**a Myahudi. Luka 18:12

▶️ Ramadan au Ramadhani
🔘 Kufunga ni moja ya nguzo 5 za Uislamu
🔘 Mwislamu mzima, mwenye afya nzuri, anatakiwa kushiriki katika swaumu (29/30)
🔘 Shabaan na Rajaab (60)
🔘 Alhamisi na Jumatatu (4x12 =48)
⚫️ Jumla kwa mwaka siku 138

⚠️ Dhibiti Uzito uliopindukia.
Fanya mazoezi ya Viungo; vijana >dk60, na wazee >dk30 kila siku. Fuata maelekezo ya wataalam usifanye kiholela.

⚠️ Usivute sigara wala kukaribia moshi wa sigara 🚭

⚠️ Usitumie pombe/vilevi 🥃.
Vilevi huchochea sukari, shinikizo la damu, hitilafu ya umeme wa moyo, nk.
Mwanaume

20/08/2024

: Rafiki

Upendo ni Lazima, Lakini Urafiki ni Machaguo Sahihi !

Rafiki Anaweza Kuwa Kikwazo; Rafiki Anaweza kuwa Kifaa !

Mpende Kila Mtu, Usimfanye Kila Mtu Rafiki !

Siyo Kila Mtu Unayempoteza ni Hasara; Chagua Anayekufanya Ukue, Tumia Akili !

Chanzo: Mchapishaji wetu





Kutoa Elimu Sahihi ya Sayansi ya Mahusiano na Kukomesha Kasumba kwenye Jamii
( Mwalimu Bora Daima efforts to educate society on science of relationships and eradicate misconceptions (conscious and subconscious) https://www.facebook.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima; https://www.instagram.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima)

03/05/2024

: Lugha Yako, Kipaji Chako

Ipo Kasumba kwa Wazazi Kuaminishwa Kwamba Mtoto Kuzungumza Lugha za Kigeni k**a vile Kiingereza, Kifaransa, Kichina, Kiarabu, nk ndiyo Uthibitisho wa Akili na Maendeleo sahihi ya kipaji chake.

Upotoshaji huu umepelekea Mtoto Kuhitimu Chuo Wakati Huo Hajiwezi na Amepoteza Uwezo Wake wa Asili wa akili, kufikiri na kipaji.

Matumizi ya Lugha za Kigeni Kujaribu Kuelemisha Vizazi ni Kuharibu Uwezo wa Watoto Kujitambua na Kupoteza Vipaji Asilia. Matumizi ya Lugha za Kigeni Yanadumaza Makuzi Sahihi ya Ubongo hususan pale Lugha Mpya [lugha Isiyotumika Mazingira Yanayomzunguka Mtoto] Inapotambulishwa katika Umri kati ya Miaka 10 mpaka 16. Katika Kipindi hiki sehemu inayopokea lugha mpya inakuwa imekomaa hivyo mtoto kutoimudu lugha na kutomudu kufikiri kupitia hiyo lugha.

Michezo ni Elimu, Burudani, Ajira, Afya, Taaluma, Maadili (Malezi), Tamaduni, n.k.

Kutambua na Kulea Kipaji cha mtoto ni Muhimu kwa Ustawi wa Maadili yetu, Kukuza Kiwanda cha Michezo na ajira, na Kutengeneza Umma Unaoelimika, Kuthamini Desturi ya Asili Yetu na kukuza uchumi wa taifa.

Chanzo: Mchapishaji wetu








Kukuza Vipaji na Kukomesha Kasumba kwenye Jamii
( Mwalimu Bora Daima efforts to identify and develop talents, and eradicate conscious and subconscious misconceptions https://www.facebook.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima; https://www.instagram.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima)

05/04/2024

: Lea Kipaji cha Mtoto

Mtoto kupewa fursa ya kuonyesha kipaji chake na kushiriki katika michezo humsaidia katika makuzi ya akili; kupata maarifa sahihi asilia, uwezo wa kuboresha stadi (kufikiri, kufanya kazi na kujitambua) na maadili mema.

Michezo ni Elimu, Burudani, Ajira, Afya, Taaluma, Maadili (Malezi), Tamaduni, n.k.

Kutambua na Kulea Kipaji cha mtoto ni Muhimu kwa Ustawi wa Maadili yetu, Kukuza Kiwanda cha Michezo na ajira, na Kutengeneza Umma Unaoelimika, Kuthamini Desturi ya Asili Yetu na kukuza uchumi wa taifa.

Chanzo: Mchapishaji wetu








Kukuza Vipaji na Kukomesha Kasumba kwenye Jamii
( Mwalimu Bora Daima efforts to identify and develop talents, and eradicate conscious and subconscious misconceptions https://www.facebook.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima; https://www.instagram.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima)

04/04/2024

: Ustawi wa Familia

Umejifunza nini kuhusu njia zinazoeneza magonjwa ya zinaa hususan Ukimwi?

Umejifunza nini kuhusu taasisi familia na mchango wake katika mmomonyoko wa maadili kwenye jamii?

Tuandikie mtazamo wako kuhusu Ustawi na Afya ya Jamii!!!

Chanzo: Mchapishaji Wetu





Kukomesha Kasumba
( Mwalimu Bora Daima efforts to eradicate conscious and subconscious misconceptions https://www.facebook.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima; https://www.instagram.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima)

 : Mwalimu HaibaShabaha ya elimu ni kuzalisha vijana wenye uwezo wa kujitegemea, wanaopewa maarifa sahihi ya kuwawezesha...
12/09/2023

: Mwalimu Haiba

Shabaha ya elimu ni kuzalisha vijana wenye uwezo wa kujitegemea, wanaopewa maarifa sahihi ya kuwawezesha kuacha utegemezi.

Mwalimu kusimamia mtihani namna hii anakuwa hana imani na wanafunzi, hajiamini, anapenda kazi yake au elimu inayotolewa ni mbovu?

Uliwahi kusimamiwa mtihani na mwalimu akichungulia madirishani au kupanda juu ya meza au dawati?
Ilikuwaje? Tueleze

Unapata elimu gani mwalimu anaposimamia mtihani namna hiyo?

Unafikiri ni kwanini mwalimu na mwanafunzi wanatumia nguvu nyingi zaidi wakati wa mtihani kuliko nguvu wanayoitumia darasani?

Je, Elimu Kupitia Lugha ya Kiingereza (lugha ya mkoloni) Inawawezesha Vijana kujitegemea wakati wa mtihani?

Je, Elimu Kupitia Lugha ya Kiingereza (lugha ya mkoloni) Inazalisha vijana wenye uwezo wa Kujitegemea maishani mwao hapa nchini?

Je, vijana wanayo haki na uhuru wa kuamua lugha inayowapima uelewa wao?

Je, vijana kupewa haki yao ya kupata elimu (kwenda shuleni), wanapewa uhuru wa kupata elimu (uhuru wa kujifunza)?

Chanzo: Mchapishaji Wetu





Kukomesha Kasumba
( Mwalimu Bora Daima efforts to eradicate conscious and subconscious misconceptions https://www.facebook.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima; https://www.instagram.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima)

 : Laana ya AfrikaUnafundisha Wanafunzi Wamfahamu Waziri Mkuu wa Canada ili Iweje?Ubongo unajazwa upuuzi usiowasaidia wa...
25/08/2023

: Laana ya Afrika

Unafundisha Wanafunzi Wamfahamu Waziri Mkuu wa Canada ili Iweje?

Ubongo unajazwa upuuzi usiowasaidia watoto na vijana kujitambua na kumdu mazingira yao.

Sera ya Elimu na Mitaala ya Elimu Inazalisha Kundi Kubwa la Watoto na Vijana Waliopata Fursa ya Kuhudhuria Shule Kupoteza Muda badala ya Kuelimika. Tubadili uelekeo na mtazamo (Language Policy and Curricula should shift focus towards sustainable livelihoods and community development through creating educated populations).

Tuzalishe watoto na vijana wenye uwezo wa kufikiri (...critical and creative thinkers) badala ya kuzalisha watoto na vijana wenye uhafifu wa kufikiri (deficit thinkers).

Hoja zote zinazotolewa kuendelea na mfumo huu unaoharibu watoto na vijana ni Sababu za (... arguments provided are ).

Sababu za Kikoloni (colossal) zinafanya mtu awe TEGEMEZI KIFIKRA (... perpetuates KNOWLEDGE DEPENDENCY).

Wasomi na wabobevu wana kasumba hii ya utegemezi wa fikra vichwani mwao kwamba bila mambo kutoka magharibu au mashariki ya mbali huwezi kuelimisha umma na kupata Maendeleo. Wanaandaa na Kusimamia Sera zenye Mwelekeo Huu.

Wanasahau Kuwa ambao ndiyo mfano wa kwenye mapinduzi ya Maendeleo (elimu, kilimo, utalii, nk) (Big Results Now _BRN) wanaelimisha watu wao kwa lugha yao ya MALAY.

Unataka kuwa k**a lakini Unaelimisha Watu wako Kupitia badala ya jambo ambalo haliwezekani uwe k**a Malaysia wanatumia ambayo ni lugha ya taifa na yenye wazungumzaji wengi inayobeba utamaduni wao na maono yao.

Wasomi, Wabia wa Maendeleo kupitia Masharti ya Mikataba, Ukosefu wa Utashi wa Kisiasa, n.k ni miong’oni mwa makundi yanayotumika kudhoofisha Waafrika wenzao wawe wajinga ili wao wanufaike na ujinga wa wenzao.

Nchi zote zilizoendelea duniani wanafundisha watu wao mambo yanayowahusu na wanaelimisha watu wao kupitia lugha zao. Huwezi Kuelimika wala Kuelimisha Jamii nzima Kupitia Lugha ya Kigeni. Lugha ni utamaduni, huwezi kupata elimu kupitia utamaduni Usio wa misingi yako. Sera na Mitaala ya Elimu ndiyo laana ya Afrika

Chanzo: Mchapishaji Wetu





Kukomesha Kasumba
( Mwalimu Bora Daima efforts to eradicate conscious and subconscious misconceptions https://www.facebook.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima; https://www.instagram.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima)

 : Eneo la Kifo; Usitumbue ChunusiJe wajua? Pokea maarifa!!!Wale Msiopenda Kuona Chunusi Usoni Acheni Mara Moja Kutumbua...
08/08/2023

: Eneo la Kifo; Usitumbue Chunusi

Je wajua? Pokea maarifa!!!

Wale Msiopenda Kuona Chunusi Usoni Acheni Mara Moja Kutumbua Chunusi hasa eneo la pembetatu - eneo la kifo, zingatieni hili vinginevyo mtakufa kwa kukosa Maarifa!

Ukipata chunusi eneo hilo iache (ziache) au pata matibabu sahihi, usijaribu kutumbua “Ni Hatari kwa Uhai Wako”!!!

Wataalamu wanaita eneo hilo lililoonyeshwa kwa pembe tatu “ENEO LA KIFO” 'Danger triangle' au 'Triangle of death'.
Eneo hilo lina mishipa ya damu ambayo huwa inakwenda moja kwa moja kwenye ubongo.

Ukitumbua chunusi eneo hilo ni rahisi sana maambukizi kufika kwenye ubongo na kukuletea majipu kwenye ubongo ambayo yanaweza kukuuwa.

KAMWE, narudia tena KAMWE, usitumbue chunusi yoyote eneo hilo lililoonyeshwa kwa pembe tatu, UTAKUFA !!!

Je, ulikuwa unafahamu maarifa haya?

Ujinga ni mzigo, kazi yetu ni kukutua mzigo wa ujinga kichwani mwako.

Chanzo: Mchapishaji Wetu, Dkt. Paul.





Kukomesha Kasumba
( Mwalimu Bora Daima efforts to eradicate conscious and subconscious misconceptions https://www.facebook.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima; https://www.instagram.com/mwalimu.bora.daima | .bora.daima)

Address

Box 11184
Mwanza
33120

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwalimu Bora Daima posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mwalimu Bora Daima:

Share