DIT Mwanza Campus

DIT Mwanza Campus Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from DIT Mwanza Campus, Science, Technology & Engineering, ILEMELA, AIRPORT Road, Mwanza.

07/06/2026

DIT MWANZA YATOA ELIMU YA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA, WANAFUNZI WATAKIWA KUTOA TAARIFA MAPEMAWanafunzi  wa Taasisi ya T...
06/06/2026

DIT MWANZA YATOA ELIMU YA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA, WANAFUNZI WATAKIWA KUTOA TAARIFA MAPEMA

Wanafunzi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza leo, tarehe 6 Juni 2026, wamepatiwa elimu kuhusu kinga na namna ya kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia kupitia semina iliyofanyika katika viwanja vya kampasi hiyo, ikihusisha wataalamu kutoka Hospitali ya Sekou Toure, Dawati la Jinsia pamoja na Jeshi la Polisi Kirumba.

Akifungua semina hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa DIT Kampasi ya Mwanza na Mratibu wa Dawati la Jinsia wa Mradi wa EASTRIP, Bi. Doris Ngogo, amesema kuwa utoaji wa elimu hiyo ni muhimu kutokana na mwingiliano wa watu wenye malezi na mitazamo tofauti chuoni.
"Tutaendelea kutoa elimu hii ili kujenga mazingira salama ya kujifunzia na kufanya kazi, huku tukiwahamasisha wanafunzi kutoa taarifa mapema wanapokumbana na vitendo vya ukatili," amesema Bi. Ngogo.

Akizungumza kwa niaba ya Kituo cha Pamoja cha (One Stop Center) Afisa Ustawi wa jamii kutoka Hospitali ya Sekou Toure, Bwana Salum Mwanaki ameleza kuwa wahanga wa ukatili wanaweza kupata huduma zote muhimu katika eneo moja ikiwemo matibabu, msaada wa kisaikolojia, ustawi wa jamii, usaidizi wa kisheria na huduma za Polisi Rafiki.

Dkt. Charles Makoye amewasisitiza wanafunzi kutafuta huduma za kitabibu haraka baada ya kufanyiwa ukatili.
"Mtu anayefanyiwa ukatili wa kingono anapaswa kufika hospitali ndani ya saa 72 ili kupata tiba na kinga dhidi ya maambukizi mbalimbali ikiwemo VVU," amesisitiza.

Naye Leah Ogutu Polisi rafiki kutoka Kituo cha Polisi Kirumba amewahimiza wanafunzi kutovumilia vitendo vya ukatili na kutoa taarifa bila hofu.

Wakizungumza kwa niaba ya wanafunzi, Notorian Nicholaus na Vivian Reuben wameishukuru Menejimenti ya DIT kwa kuandaa semina hiyo, wakieleza kuwa imewaongezea uelewa kuhusu haki zao na namna ya kujikinga dhidi ya vitendo vya ukatili.
"Tumejifunza umuhimu wa kutoa taarifa mapema na kutafuta msaada bila kuogopa. Elimu hii itatusaidia kufanya maamuzi sahihi katika maisha yetu ya chuoni," wamesema.

Karibu Uombe Dirisha la Udahili awamu ya kwanza lipo wazi omba kupitia link hapo juu kusoma kozi zenye Fursa ya mkopo wa...
06/06/2026

Karibu Uombe Dirisha la Udahili awamu ya kwanza lipo wazi omba kupitia link hapo juu kusoma kozi zenye Fursa ya mkopo wa serikali

KANALI MSTAFU SIMBAKALIA AFURAHISHWA NA MAENDELEO YA MRADI WA CELPAT DITMwenyekiti wa Kamati ya Ushauri Viwandani ya Mra...
05/06/2026

KANALI MSTAFU SIMBAKALIA AFURAHISHWA NA MAENDELEO YA MRADI WA CELPAT DIT

Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri Viwandani ya Mradi wa CELPAT, Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia, leo tarehe 5 Juni 2026 ametembelea DIT kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu ya kufundishia na kujifunzia inayotekelezwa chini ya mradi huo.

Katika ziara hiyo, ametembelea maabara nane (8) za kisasa, karakana ya uchakataji wa ngozi na kiwanda cha kisasa cha kutengeneza bidhaa za ngozi, ambapo ameonesha kuridhishwa na hatua kubwa iliyofikiwa. Amesema maendeleo hayo yanatimiza ndoto za Watanzania na wadau wa elimu za kuona DIT ikizalisha wataalamu na bidhaa za ngozi zenye ubora wa viwango vya kimataifa.

Kanali Simbakalia pia amefurahishwa na kuanza kutumika kwa ofisi mbalimbali katika majengo mapya, jambo linaloonesha utayari wa DIT kutumia kikamilifu miundombinu iliyowekezwa kwa ajili ya maendeleo ya elimu na viwanda.

Aidha, amempongeza Mkurugenzi wa Kampasi, Dkt. John A. Msumba, kwa usimamizi mzuri wa mradi huo na juhudi zake katika kuhakikisha uwekezaji huo unaleta matokeo chanya kwa taasisi na taifa kwa ujumla.

WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI PASIANSI WAVUTIWA NA UBUNIFU NA TEKNOLOJIA DIT MWANZAWanafunzi wa Shule ya Sekondari Pas...
05/06/2026

WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI PASIANSI WAVUTIWA NA UBUNIFU NA TEKNOLOJIA DIT MWANZA

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Pasiansi wamefanya ziara ya kimafunzo kwa vitendo katika Kampasi ya DIT Mwanza kwa lengo la kujifunza teknolojia mbalimbali, ubunifu na fursa za masomo zinazotolewa na Taasisi hiyo.

Ziara hiyo imewapa wanafunzi nafasi ya kuona kwa karibu namna elimu ya sayansi na teknolojia inavyotumika kutatua changamoto za kijamii na kiuchumi.

Katika ziara hiyo, wanafunzi wametembelea karakana za uchakataji wa ngozi na utengenezaji wa viatu ambapo wamejifunza hatua mbalimbali za uzalishaji wa bidhaa za ngozi kuanzia malighafi hadi bidhaa kamili.

Pia wamepata fursa ya kushuhudia kazi za ubunifu zinazofanywa na wanafunzi na wataalamu wa DIT katika kuongeza thamani ya mazao ya ngozi nchini.

Aidha, wanafunzi hao wametembelea maabara za sayansi pamoja na maabara za kompyuta, ambapo wamejionea vifaa vya kisasa vinavyotumika katika mafunzo na tafiti za kiteknolojia. Wakiwa katika maabara hizo, wamepata maelezo kuhusu matumizi ya teknolojia katika sekta mbalimbali ikiwemo viwanda, afya, mawasiliano na biashara.

Akizungumza baada ya ziara hiyo, mmoja wa wanafunzi wa Pasiansi, Neema John, amesema kuwa amevutiwa na mazingira ya kujifunzia yaliyopo DIT Mwanza na ubunifu unaofanywa na wanafunzi wake. "Ziara hii imeniongezea hamasa ya kusoma masomo ya sayansi na teknolojia.Nimejifunza mambo mengi ambayo sikuwa nayafahamu kuhusu uchakataji wa ngozi na matumizi ya teknolojia katika kutatua changamoto za jamii," alisema.

Kwa upande wake, mwanafunzi mwingine, Brian Magesa, amesema kuwa ziara hiyo imewasaidia kuona fursa mbalimbali zilizopo katika elimu ya ufundi na teknolojia. "Tumepata uzoefu wa kipekee kwa kuona maabara na karakana za kisasa. DIT Mwanza ni sehemu inayowapa vijana nafasi ya kubuni na kutengeneza suluhisho za changamoto zinazotuzunguka, jambo ambalo limetutia moyo kuendelea kufanya vizuri katika masomo yetu," amesema.

WANAFUNZI WA DIT MWANZA WAPATA UZOEFU WA KIPEKEE BUNGENI DODOMA.Wanafunzi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) K...
02/06/2026

WANAFUNZI WA DIT MWANZA WAPATA UZOEFU WA KIPEKEE BUNGENI DODOMA.

Wanafunzi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza, leo tarehe 2 Juni 2026, wamefanya ziara ya mafunzo kwa vitendo katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma kwa mwaliko wa Mbunge wa Jimbo la Ilemela, Mhe. William Kafiti.

Ziara hiyo imelenga kuwawezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo namna Bunge linavyotekeleza majukumu yake ya kikatiba, hususan mchakato wa kujadili na kupitisha bajeti pamoja na kuwasilisha na kujadili hoja mbalimbali za maendeleo ya taifa.

Wakiwa bungeni, wanafunzi hao wamepata fursa ya kushiriki kikao kilichohusisha maswali na majibu ya wabunge kuelekea mwaka mpya wa fedha 2026/2027, jambo lililowapa uelewa mpana kuhusu mifumo ya uongozi na utungaji wa maamuzi ya kitaifa.

Mbali na kutembelea Bunge, wanafunzi hao pia wametembelea vivutio mbalimbali vya jijini Dodoma na kufanya ziara katika shule za sekondari ambapo wamehamasisha wanafunzi kujiunga na masomo ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati (STEM) kwa ajili ya kujenga taifa lenye wataalamu wa teknolojia na ubunifu.

Ziara hiyo imechangia kuongeza maarifa ya kitaaluma, kuimarisha mtazamo wa wanafunzi kuhusu mazingira ya kazi baada ya masomo na kuwajengea uwezo wa kuunganisha nadharia wanazojifunza darasani na uhalisia wa utekelezaji wa majukumu katika taasisi mbalimbali za umma.
TechnologyForDevelopment

WANAFUNZI WA DIT MWANZA WAHAMASISHA ELIMU YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA.Wanafunzi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT...
01/06/2026

WANAFUNZI WA DIT MWANZA WAHAMASISHA ELIMU YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA.

Wanafunzi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza wamefanya ziara kutoka Mwanza hadi Dodoma iliyowapa fursa ya kujifunza, kujitangaza kitaaluma na kuhamasisha vijana kuhusu umuhimu wa elimu ya sayansi na teknolojia.

Katika ziara hiyo, wanafunzi hao wametembelea shule za sekondari ikiwemo Ziba sekondari (Tabora), Muhalala (Singida), Dodoma Sekondari, Viwandani, Kikuyu, Mkonze na Wela za jijini Dodoma ambapo wametoa elimu kuhusu fursa za masomo zinazotolewa na DIT na kuwahamasisha wanafunzi kuchagua masomo ya sayansi kwa ajili ya kujenga taifa lenye wataalamu wa teknolojia na ubunifu.

Wakiwa katika shule hizo, wameeleza fursa mbalimbali zinazopatikana chuoni ikiwemo mikopo ya elimu ya juu inayotolewa na Serikali pamoja na nafasi za ajira na kujiajiri kupitia taaluma za teknolojia, uhandisi na ubunifu.

Aidha, wanafunzi hao wametembelea mabanda ya maonesho katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira yanayofanyika katika Viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Centre (JKCC) jijini Dodoma, ambapo wamepata fursa ya kujifunza teknolojia na ubunifu mbalimbali vinavyotumika katika uhifadhi wa mazingira na maendeleo endelevu.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, mwanafunzi wa DIT Mwanza, Vivian Leuben amesema: “Tumefurahi kupata nafasi ya kuwa mabalozi wa DIT kwa kuwafikia wanafunzi wa shule za sekondari na kuwaeleza fursa zilizopo.
Tunaamini elimu ya sayansi na teknolojia ndiyo njia muhimu ya kufikia maendeleo ya taifa na kutatua changamoto za jamii.”

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI RUSUMO NEW VISION WATEMBELEA DIT MWANZA KUJIFUNZA TEKNOLOJIA NA UBUNIFUWanafunzi wa Shule y...
30/05/2026

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI RUSUMO NEW VISION WATEMBELEA DIT MWANZA KUJIFUNZA TEKNOLOJIA NA UBUNIFU

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Rusumo New Vision kutoka Wilaya ya Ngara, Mkoa wa Kagera, wamefanya ziara ya mafunzo kwa vitendo katika Kampasi ya DIT Mwanza kwa lengo la kujifunza shughuli mbalimbali za kiteknolojia na ubunifu zinazotekelezwa na Taasisi hiyo.

Katika ziara hiyo, wanafunzi walipata fursa ya kutembelea maabara mbalimbali na kujifunza kuhusu teknolojia ya uchakataji bidhaa za ngozi yaani (Leather Processing technology), pamoja na shughuli nyingine za maabara zinazohusiana na sayansi, teknolojia na ubunifu.

Aidha, walijionea bunifu mbalimbali zinazotengenezwa na walimu na wanafunzi wa DIT, zikiwemo bidhaa za ngozi na teknolojia zinazolenga kutoa suluhisho kwa changamoto za kijamii na kiuchumi.

Ziara hiyo imewasaidia wanafunzi kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa elimu ya sayansi, teknolojia na ubunifu katika kujenga taifa lenye uchumi wa viwanda na kuongeza hamasa ya kufuatilia taaluma za kiufundi na teknolojia katika ngazi za juu za elimu.

FutureInnovators DITTanzania

DIRISHA LA UDAHILI LIPO WAZI 2026/2027Kuanzia tarehe 28 Mei hadi 10 Julai, 2026Omba kujiunga na programu za Astashahada ...
30/05/2026

DIRISHA LA UDAHILI LIPO WAZI 2026/2027

Kuanzia tarehe 28 Mei hadi 10 Julai, 2026

Omba kujiunga na programu za Astashahada na Stashahada katika fani za:

Fashion Design Technology
Textile Technology
Agro Post Harvest Technology
Agro Bio Process Technology
Food Processing Technology
Science and Laboratory Technology
Leather Processing Technology
Leather Products Technology
Information Technology (IT)

Omba kupitia:
🔗 https://admission.dit.ac.tz/admission/apply⁠�
Kwa maelezo zaidi:
📞 0625 833 819
📞 0629 153 727
📞 0754 660 773

WANAFUNZI WABUNIFU WA DIT MWANZA WANG’ARA TANZANIA TUWEKEZE FORUM 2026.Wanafunzi Taasisi ya Teknolojia Dar es salaam DIT...
29/05/2026

WANAFUNZI WABUNIFU WA DIT MWANZA WANG’ARA TANZANIA TUWEKEZE FORUM 2026.

Wanafunzi Taasisi ya Teknolojia Dar es salaam DIT Kampasi ya Mwanza wabunifu wameonyesha uwezo mkubwa wa ubunifu na ujasiriamali kupitia ushiriki wao katika Kongamano la siku mbili la Tanzania Tuwekeze Forum 2026, lililozinduliwa rasmi tarehe 28 Mei 2026 likiwakutanisha wadau mbalimbali wa uwekezaji, viwanda na maendeleo ya biashara.

Kongamano hilo limehusisha zaidi ya washiriki 200 wakiwemo wawekezaji, wajasiriamali, wamiliki wa viwanda, waajiri, taasisi za kifedha, wanataaluma na wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali vya kanda ya ziwa, pamoja na taasisi na wizara muhimu k**a Wizara ya Fedha, Wizara ya Uwekezaji na UNDP.

Katika jukwaa hilo, wanafunzi wa DIT Mwanza walipata nafasi ya kuwasilisha bunifu zao za kiteknolojia na kibiashara, hatua iliyovutia wadau kutokana na ubunifu na uwezo wa mawazo hayo kutoa suluhisho katika jamii na kuongeza thamani ya bidhaa na huduma.

Miongoni mwa washiriki ni Ashrafu Maranda, Waziri wa "Teaching Factory" wa DIT, ambaye amesisitiza umuhimu wa serikali kuongeza uwekezaji katika sekta ya ngozi ili kuimarisha mnyororo wa thamani wa mazao ya ngozi nchini.
“Sekta ya ngozi ina uwezo mkubwa wa kuchangia uchumi wa viwanda. Ni muhimu kuwekeza kwa wataalamu na teknolojia ili kuongeza thamani kuanzia hatua ya awali hadi bidhaa za mwisho,” amesema Ashrafu Maranda.

Ushiriki wa DIT Mwanza katika kongamano hilo unaendelea kuimarisha nafasi ya taasisi hiyo katika kukuza ubunifu, ujasiriamali na maandalizi ya wataalamu wenye ushindani katika soko la ajira na maendeleo ya taifa.

Address

ILEMELA, AIRPORT Road
Mwanza

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30
Saturday 07:30 - 15:30
Sunday 07:30 - 15:30

Telephone

+255738204060

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when DIT Mwanza Campus posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to DIT Mwanza Campus:

Share