DIT Mwanza Campus

DIT Mwanza Campus Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from DIT Mwanza Campus, Science, Technology & Engineering, ILEMELA, AIRPORT Road, Mwanza.

DIT MWANZA YAFANYA MAFUNZO YA UWEZESHAJI WANAWAKE NA UONGOZIWanawake watumishi pamoja na wanafunzi wa k**e wa Taasisi ya...
11/05/2026

DIT MWANZA YAFANYA MAFUNZO YA UWEZESHAJI WANAWAKE NA UONGOZI

Wanawake watumishi pamoja na wanafunzi wa k**e wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza wameshiriki semina ya siku mbili kuhusu uwezeshaji wanawake na masuala ya kijinsia (Women Empowerment in Leadership and Gender Workshop) yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kujitambua, kujiamini na kuimarisha uongozi binafsi.

Awali akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mkurugenzi wa DIT Kampasi ya Mwanza, Dkt. Msumba, Mhandisi Issa Mwangosi ameishukuru taasisi ya Dr. Angela Daalmann pamoja na washirika wake kwa uamuzi wao wa kushirikiana na DIT katika kuwawezesha wanawake kupitia mafunzo yenye tija kwa maendeleo ya jamii na taasisi.
“Tunathamini mchango mkubwa wa Dr. Angela na washirika wake katika kuwawezesha wanawake wetu kupata maarifa ya uongozi, kujiamini na kujitambua.

Mafunzo haya yanaenda kuleta chachu mpya ya maendeleo kwa washiriki wetu na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Ujerumani,” amesema Mhandisi Mwangosi.

Mafunzo hayo yanawezeshwa na Dr. Angela Daalmann kutoka Ujerumani kupitia kampuni yake ya Anda GmbH, kwa udhamini wa Serikali ya Lower Saxony State ya Ujerumani kwa kushirikiana na DIT Mwanza.

Washiriki wa semina hiyo wanapata mafunzo katika maeneo mbalimbali ikiwemo Gender Roles, Personal Leadership, Self-confidence, Positive Mindset, Thinking Straight pamoja na mbinu za kujitambua na kuthubutu katika kufikia malengo yao ya maisha na taaluma.

Aidha, mafunzo hayo yanapata ushirikiano kutoka kwa wasaidizi wa Dr. Angela ambao ni Khadija Ally kutoka STK Coaching pamoja na Yohana Misese kutoka Simiyu Sports Promotion Centre ya Bariadi.

Hatahivyo,Kupitia mafunzo hayo, DIT Mwanza inaendelea kuimarisha ushirikiano wa kimataifa kati ya Tanzania na Ujerumani sambamba na kuunga mkono agenda ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa kuhusu uwezeshaji wanawake na usawa wa kijinsia.

09/05/2026

KARIBU DIT MWANZA KITOVU CHA ELIMU YA UJUZI NA BUNIFU WA TEKNOLOJIA.

Karibu Ushuhudie mabadiliko makubwa ya DIT Kampasi ya Mwanza baada ya uwekezaji wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa zaidi ya TZS Bilioni 37 kupitia mradi wa EASTRIP, ukilenga kuimarisha elimu ya teknolojia na ufundi stadi kwa kujenga miundombinu mizuri ya Madarasa, Maabara,Karakana na Hosteli za kisasa.

Wazazi na walezi mnakaribishwa kuleta vijana wenu kwa Mhula wa Masomo 2025/2026, katika mazingira bora ya kujifunzia na fursa ya Mikopo ya Serikali (HESLB) kuanzia Cheti, Stashahada hadi Shahada ya Kwanza.

Kozi zetu pendwa:
• Bachelor of Technology in Laboratory Science

Diploma:

Fashion Design Technology | Textile Technology | Agro Post Harvest Technology | Agro Bio Process Technology | Food Processing Technology | Science & Laboratory Technology | Leather Processing Technology | Leather Products Technology | Information Technology (IT)

DIT Mwanza – Teknolojia kwa Maendeleo na Ajira za Kesho.

Bajeti ya Wizara ya Elimu 2026/27
07/05/2026

Bajeti ya Wizara ya Elimu 2026/27

MWANAFUNZI WA DIT ENOS LAURENT WA KWANZA KULIA AIBUKA MSHINDI WA PILI SHINDANO LA CLIMATHON MWANZA 2026 Mwanafunzi wa DI...
05/05/2026

MWANAFUNZI WA DIT ENOS LAURENT WA KWANZA KULIA AIBUKA MSHINDI WA PILI SHINDANO LA CLIMATHON MWANZA 2026

Mwanafunzi wa DIT Kampasi ya Mwanza, Enos Laurent Kiyogela, anayesoma mwaka wa kwanza katika kozi ya Teknolojia ya Ubunifu na mitindo, ameibuka mshindi wa pili katika shindano la Climathon Mwanza 2026 lililofanyika katika ukumbi wa Next Hub.

Katika shindano hilo, Enos aliwasilisha ubunifu wake unaojulikana k**a “Weeds to Wealth,” unaolenga kukabiliana na changamoto ya magugu maji yanayoathiri mazingira ya Ziwa Victoria kwa kuyageuza kuwa rasilimali zenye thamani. Kupitia ubunifu huu, magugu hayo hutumika kuzalisha mkaa mbadala, mbolea ya asili, pamoja na bidhaa za samani k**a viti.

Ubunifu huu una manufaa makubwa kwa jamii, ikiwemo kupunguza utegemezi wa ukataji miti kwa ajili ya mkaa, kuboresha mazingira ya ziwa na hivyo kusaidia maisha ya viumbe hai, hususan samaki, pamoja na kutoa mbolea rafiki kwa shughuli za kilimo. Aidha, unafungua fursa za ajira na kuongeza kipato kwa jamii zinazozunguka ziwa.

Mafanikio haya yanaakisi mchango wa DIT katika kukuza ubunifu unaolenga kutoa suluhisho endelevu kwa changamoto za kijamii na kimazingira.

WATUMISHI WA DIT MWANZA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA MEI MOSI MISUGWIWatumishi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) ...
01/05/2026

WATUMISHI WA DIT MWANZA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA MEI MOSI MISUGWI

Watumishi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza leo, Mei 1, 2026, wameshiriki maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika kimkoa wilayani Misugwi, sambamba na taasisi mbalimbali za umma na binafsi.

Maadhimisho ya mwaka huu yameongozwa na kaulimbiu: "Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050".

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, amesisitiza: “Wafanyakazi ni nguzo ya maendeleo ya Taifa; nidhamu, ubunifu na uwajibikaji viende sambamba na juhudi za kujenga uchumi imara.”

Aidha, mkuu huyo wa mkoa amehimiza kuimarishwa kwa mazingira bora ya kazi na kuongeza tija katika uzalishaji.

Ushiriki wa DIT Mwanza umeakisi dhamira ya taasisi hiyo katika kuunga mkono juhudi za Serikali za kuendeleza rasilimali watu, kukuza ubunifu wa kiteknolojia na kuimarisha mchango wa sekta ya elimu katika uchumi wa viwanda.

DIT inaendelea kuthamini mchango wa watumishi wake katika kuimarisha huduma, ubunifu na maendeleo ya Taifa.

Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza inawatakia watumishi wake pamoja na wafanyakazi wa taasisi m...
30/04/2026

Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza inawatakia watumishi wake pamoja na wafanyakazi wa taasisi mbalimbali Heri ya Siku ya Wafanyakazi Duniani. Tunathamini mchango wenu katika kuendesha shughuli za umma, kuimarisha huduma na kuchochea maendeleo ya Taifa. Endeleeni kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na kujituma.

MWENYEKITI WA BARAZA LA UONGOZI LA  NACTVET AIPONGEZA DIT MWANZA KWA UBORA WA MAFUNZO YA VITENDO.Leo tarehe 28 Aprili 20...
28/04/2026

MWENYEKITI WA BARAZA LA UONGOZI LA NACTVET AIPONGEZA DIT MWANZA KWA UBORA WA MAFUNZO YA VITENDO.

Leo tarehe 28 Aprili 2026, Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la NACTVET, Bi. Bernadetta N. Ndunguru, ametembelea DIT Kampasi ya Mwanza katika ziara ya kanda ya Ziwa kukagua usimamizi wa elimu ya ufundi stadi, ikiwemo Kituo cha Umahiri wa Ngozi.

Amepongeza utekelezaji wa dhana ya Teaching Factory kwa kuwawezesha wanafunzi kupata ujuzi wa vitendo unaoendana na mahitaji ya viwanda, amesema, “Mfumo huu unaongeza ushindani wa wahitimu wetu katika soko la ajira.”

Pia ameipongeza DIT kwa kufanya tafiti za Tracer Study zinazosaidia kufuatilia ajira za wahitimu na kuoanisha mitaala na soko la ajira, akizitaka taasisi nyingine kujifunza kutoka kwao.

Aidha, ameridhishwa na kozi za Agro Post-Harvest Technology akieleza kuwa zitasaidia kupunguza hasara kwa wakulima, huku akiipongeza taasisi hiyo kwa miundombinu ya kisasa iliyoboreshwa kupitia mradi wa EASTRIP.

DIT MWANZA YANG’ARA KATIKA KONGAMANO LA MWANAMKE WA  ILEMELATaasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza ...
25/04/2026

DIT MWANZA YANG’ARA KATIKA KONGAMANO LA MWANAMKE WA ILEMELA

Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza imeshiriki kikamilifu katika Kongamano la Siku ya Mwanamke Wilaya ya Ilemela lililofanyika leo, Aprili 25, 2026, ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima (Mb), aliyewakilishwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda.

Katika hotuba yake, Mhe. Mtanda amesisitiza kuwa mwanamke imara ni msingi wa uchumi imara, akihimiza wanawake kutumia vyema fursa zilizopo kujijengea uwezo wa kiuchumi kwa manufaa ya familia na taifa.

Katika kongamano hilo lililojumuisha utoaji wa mikopo, elimu ya ujasiriamali na maonesho ya bidhaa, DIT Mwanza imeshiriki k**a mdhamini pamoja na kushiriki katika maonesho ya ubunifu. Taasisi imewasilisha bidhaa na bunifu mbalimbali zilizotengenezwa na wanafunzi kutoka idara tofauti kwa kutumia ujuzi wa vitendo na miundombinu ya karakana zilizopo chuoni, hatua iliyoonesha mchango wa elimu ya ufundi katika kukuza uchumi shindani.

Bidhaa hizo zimevutia kwa kiwango kikubwa wazazi, wadau wa elimu na washiriki wengine wa kongamano, waliopata fursa ya kujifunza kuhusu ubora na thamani ya mafunzo yanayotolewa na DIT. Sambamba na hilo, wadau wamepatiwa taarifa kuhusu fursa za mikopo ya Serikali kwa wanafunzi wanaochagua kusoma DIT, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza upatikanaji wa elimu ya ufundi na stadi za kazi zenye tija.

Aidha, katika uwakilishi wake, DIT imesimamiwa na Afisa Rasilimali Watu, Bi. Alice Mwasyoge, aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Kampasi, Dkt. John Msumba.

Hatahivyo, ushiriki huo umeendelea kuimarisha nafasi ya taasisi katika kushirikiana na jamii na wadau mbalimbali katika kukuza ujuzi, ubunifu na uwezeshaji wa wanawake kiuchumi.

DIT MWANZA YAKUSANYA MAONI YA WADAU KUANDAA MITAALA YA MIPYA YA SHAHADA YA  NGOZI NA SAYANSI YA CHAKULALeo, tarehe 23 Ap...
23/04/2026

DIT MWANZA YAKUSANYA MAONI YA WADAU KUANDAA MITAALA YA MIPYA YA SHAHADA YA NGOZI NA SAYANSI YA CHAKULA

Leo, tarehe 23 Aprili 2026, Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza imeendesha zoezi la kukusanya maoni kutoka kwa wadau wa sekta ya ngozi na sayansi na teknolojia ya chakula, likilenga kuandaa mitaala mipya ya Shahada ya Teknolojia ya Sayansi ya Chakula na Shahada ya Uhandisi katika Teknolojia ya Ngozi.

Mgeni rasmi katika tukio hilo alikuwa Naibu Mkuu wa Taasisi anayeshughulikia Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu, Prof. Ezekiel Amri, ambaye amesisitiza umuhimu wa kuandaa programu zitakazozalisha wataalamu wenye ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la ajira na kuchochea maendeleo ya viwanda.
“Ni wajibu wetu kuhakikisha mitaala hii inazingatia uhalisia wa mahitaji ya soko na kuongeza thamani ya rasilimali tulizonazo ili kuzalisha wataalamu wenye ujuzi wa vitendo,” amesema Prof. Amri.

Akizungumza katika zoezi hilo, amebainisha kuwa DIT Mwanza ni kituo cha umahiri katika teknolojia ya ngozi, na kuanzishwa kwa programu hizo kutachangia kuongeza thamani ya rasilimali za mifugo nchini, ambapo Tanzania ina idadi kubwa ya mifugo na sehemu kubwa ya wananchi hutegemea sekta hiyo kiuchumi.

Washiriki wamehamasishwa kutoa maoni yao kupitia dodoso maalum ili kuboresha mitaala hiyo, kwa lengo la kuimarisha ujuzi wa vitendo, kuongeza thamani ya mazao, na kuandaa wataalamu watakaoweza kushindana kikanda na kimataifa.

Pure leather Products Manufacutred from DIT Mwanza Campus
21/04/2026

Pure leather Products Manufacutred from DIT Mwanza Campus

DIT YAENDESHA MAFUNZO YA UBORA WA CHAKULA NA BIDHAA ZA NGOZI,KWA WAJASIRIMALI MWANZAChama cha Ubora Tanzania (NQAT), kup...
13/04/2026

DIT YAENDESHA MAFUNZO YA UBORA WA CHAKULA NA BIDHAA ZA NGOZI,KWA WAJASIRIMALI MWANZA

Chama cha Ubora Tanzania (NQAT), kupitia Programu ya ITC MARKUP II inayofadhiliwa na Umoja wa Ulaya kwa kushirikiana na Taasisi ya Teknolojia Dar es salaam (DIT) Kampasi ya Mwanza wameandaa mafunzo maalum ya kuhusu Usalama wa Chakula (HACCP), Usimamizi wa Ubora (QMS), na Kanuni za Lean.

Mafunzo haya yanalenga kuongeza fursa za masoko kwa wasindikaji na wauzaji nje katika minyororo ya thamani ya ngozi, viungo, kahawa, parachichi na kakao.

Aidha,mkazo umewekwa kwenye sekta za viungo na ngozi
huku washiriki wa mafunzo hayo wakiwa ni, wajasiriamali wadogo na wa kati (SMEs), wataalamu wa chakula na ngozi kutoka DIT, wakishirikiana na wakufunzi kutoka (NQAT) na baadhi yao wakiwa ni wataalam wa DIT.

Mafunzo haya yanafanyika kwa siku mbili: 13–14 Aprili, yakilenga kuimarisha ubora wa bidhaa ili kuongeza ushindani na upatikanaji wa masoko ya ndani na kimataifa.

Address

ILEMELA, AIRPORT Road
Mwanza

Opening Hours

Monday 07:30 - 15:30
Tuesday 07:30 - 15:30
Wednesday 07:30 - 15:30
Thursday 07:30 - 15:30
Friday 07:30 - 15:30
Saturday 07:30 - 15:30
Sunday 07:30 - 15:30

Telephone

+255738204060

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when DIT Mwanza Campus posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to DIT Mwanza Campus:

Share