Simulizi Zetu

Simulizi   Zetu Mtunzi Wetu

Stori ipo hewani hadi sehemu ya sita [ MOYO WA MASIKINI ]
31/01/2024

Stori ipo hewani hadi sehemu ya sita [ MOYO WA MASIKINI ]

MOYO WA MASIKINI 💔😢sehemu ya 6💓Simulizi page💝Usiku wa manane REHEMA alishtuka usingizini na kumuona kiba bado yupo macho...
31/01/2024

MOYO WA MASIKINI 💔😢

sehemu ya 6💓

Simulizi page💝

Usiku wa manane REHEMA alishtuka usingizini na kumuona kiba bado yupo macho , kiba alimwambia REHEMA

" wew mwanamke unakoroma k**a jenereta , usiwe na hofu lala tu nimesha ongea na kaka yako "
Ila kiba alionekana kutokuwa sawa kabisa ilimbidi rehema asogee karibu kwa kiba na kumuuliza

" yule ndio ADA mwenyewe mnaependana mbona k**a ni mke wa mtu , ila sio mbaya mimi nipo karibu yako "

Kiba alitabasamu tu sababu rehema ndio maneno yake ya kila siku ,

Siku hiyo ilipita

Siku nyingine tena kiba yupo mgahawani asubuhi na mapema akifanya usafi linakuja gari na anashuka yule jiDada wa rich anaonekana kuwa na hasira sana

Anasogea mbele ya kiba na kumpiga Kofi kwa hasira
" kwanini unakuwa kikwazo kwenye mahusiano yangu na rich"

Kiba hakulipa Kofi alimshika mkono na kumvuta sehemu waongee

" Dada yangu Leo ngojaa nikwanbie kitu , rich anamdogo wake na pia na yatima hawa ,, ndugu zao waliwatenga zamani sana , wewe una mama na baba unandugu wanao kupenda unamume tajiri na mkorofi wewe mwenyewe unamjua Leo rich akifa dogo lake ataishi maisha gani , nafanya haya sio kwamba namuonea wivu hapana , nalipa fadhila aliniokota mtaani hapa nilikuwa nikija kuomba chakula ndio maana namuona wa muhimu sana katika maisha yetu "

Waliongea mengi sana siku hiyo ilipita , inakuja Siku nyingine usiku rich akiwa njiani anarudi nyumbani alitekwa na watu wasio julikana , rehema na kiba walitafuta sana walikataa tamaa baada ya muda kupita

Rehema anapigiwa simu kutoka hospital wanaenda na kiba wanamkuta rich yupo hali mautiuti kaharibika usoni kavunjwa vunjwa mifupa anapumulia kwa machine "

Kiba alipata hasira alitoka pale hospital na kumfuata yule Dada nyumbani kwake , alifika getini alizuiliwa kuingia na mlinzi alisubiri sana mwisho gari likaonekana likitoka alilisimamisha ,

Gari lilipo shushwa vioo alionekana yule Dada akiwa na mumewe aliwasalimu na kuwaambia

" tuna shukuru hatuta kuja kuwasahau katika maisha yetu "

Siku hiyo usiku wakiwa hospitali rehema alikuwa akilia tu , alikuja yule Dada kiba alimfukuza k**a mwizi

Baadae siku nyingi kupita rich alionekana kupata hafadhali walipiga stori nyingi sana mwisho rich alimuomba kiba

" kiba naomba muangalie mdogo wangu ,k**a nisipo kuwepo sababu mnapendeza sana mkiwa pamojaa najua utawezana nae sababu huyo yupo hivyo kutokana na mazingira aliyo lelewa , muangalie vizuri ndio malipo yangu nakuomba "

Kiba hakujua aliongea hivyo kwanini alikuja rehema akiwa amebeba chakula alikuwa na furaha sana kwa sababu kaka yake amepata hafadhali rehema alienda kununua hadi shati na suruali k**a zawadi ya kaka yake akitoka hospital

Siku hiyo ilipita siku ya pili asubuhi , mungu alimchukua rich hakuna aliye fikilia wala kuzania

Rehema alikuja hospital akiwa amebeba chai na kiba alikuwa amelala pembeni , rehema alikuwa na kelele

" kaka kaka Leo , nataka nikuambie kitu "

Kiba alimkatisha njiani kwa kumwambia

" amepumzika mwache bhna"

Rehema alimuandalia chai kiba walikunywa kwa pamojaa wakipiga stori kwa kunong'ona wakipiga utani muda huo hawakujua k**a kaka yao amesha fariki 😢

Baada ya muda kidogo alikuja nesi alipomgusa rich alishtuka na kutoka nje mbio kumwita dokta kiba na REHEMA walitolewa njee wote walikuwa wamepigwa na butwa

Dokta anarudi na kuuliza nani ndugu mtu wa karibu na Richard nelsoni kiyako rich na REHEMA walijitokeza dokta aliwaitia pembeni na kuwaambia ukweli

Aise ! Ilikuwa huzuni sana rehema alilia sana 😭😭

BAADA YA MIEZI MINNE

USIKOSE SEHEMU INAYO FUATA
Tutaendelea na stori yetu usisahau kufuatilia simulizi zetu page kwa stori nyingi nyingi siuzi story zangu , mtazipata bure kabisa ninacho kihitaji kutoka kwenu ni saport tu comment ,like , share pia follow page hii ili uendelee kupata stori kwa urahisi

MOYO WA MASIKINI 💔🌹sehemu ya tano 🏵🌹Simulizi zetu page 🌷🌷Njombe tanzania🌲🌲💐REHEMA ALIKUWA AKISIKILIZA KWA KUIBIA , ALIKU...
31/01/2024

MOYO WA MASIKINI 💔🌹

sehemu ya tano 🏵🌹

Simulizi zetu page 🌷🌷

Njombe tanzania🌲🌲💐

REHEMA ALIKUWA AKISIKILIZA KWA KUIBIA , ALIKUWA AMETEGA SIKIO KWENYE MLANGO

Baada ya kiba kumpiga mkwara yule jamaa alitoka nje akiwa na hasira sana , anafika nje anamkuta rehema akaanza kumfokea

" wewe kamdomo hako katakuponza watakuja wakupige shauri yako , wewe dogo matatizo kaka nae matatizo"

Basi yaliisha kiivyo na siku ikapita , hatimaye siku nyingine REHEMA NA KIBA wanaonekana njian wakiwa wanarudi toka sokoni , muda huo alipita mwanaume akiwa anasukuma mkokoteni umesheheni mahindi mabichi🌽 KIBA akasema

" kwenye maisha ya kawaida mwanaume anapitia wakati mgumu sana "

REHEMA alidakia kwa sauti kubwa

" wewe unasema nini ? Je mwanamke anazaa "

Walikuwa wakibishana sana , ghafla mbele wakaona mtoto anataka kuvuka barabara mbele kulikuwa na gari la mizigo likija , KIBA alimkimbilia yule mtoto na kumsaidia , akiwa ameshikwa na hasira kuona ule uzembe anakuja binti kumchukua mtoto

" asante kaka amenipokonyoka nilipo kuwa dukani ,"

KIBA aliuliza " mtoto wa kwako "

" hamnaa kaka ni wa boss wangu yule pale amekaa saluni anatengeneza nywele "

KIBA alimuangalia vizuri yule boss k**a anamjua hivi , alisogea karibu kuakikisha k**a ni mwenyewe ni kweli bhana ni ADA

" BINTI ALIYE KATA TAMAA NAE AKAJUA WAMEPOTEANA "

alimfuata mfanyakazi na kumuuliza" boss wako anaitwa ADA ,"

" ndio anaitwa ADA , ameolewa na mumewe anaitwa AYUNI "

kiba alikuwa mnyonge sana REHEMA alikuwa akimsubiri kiba waondoke , akaona kiba anakawia sana akamwita kwa sauti kubwa si mnajua REHEMA ni aina ya wanawake walopokaji

" kibaaaa ! Twende bhn "

Hilo jina alilisikia ADA akiwa saloon alishtuka akaangalia nje ndio akamuona KIBA akiwa anaondoka , aliinuka haraka ila alichelewa ikambidi amuulize mfanyakazi wake

" yule kijana uliye kuwa nae anaitwa nan, na amekwambiaje "

Mfanyakazi alimjibu " anaitwa kiba na alikuulizia jina , anaonekana anakujua vizuri maana ameondoka na huzuni kweli , baada ya kujua jina lako"

KIBA wakiwa njiani alikuwa haongei " mkimya " REHEMA nae alikosa MTU wa kubishana nae wakawa wapo kimya tu

Ghafla likapita gari halafu likasimama likapiga honi walipo lifikia likashusha kioo alikuwa " alikuwa jidada wa Richard "

"Njoeni ni wape lift si mnaelekea mgahawani "

Alisema yule Dada REHEMA alitaka kukimbilia KIBA alimdaka mkono na kumjibu yule Dada

" usiwe mwema kwetu , onesha wema kwa kaka yetu , achana nae kwa ajiri ya usalama wake "

Walivyo sema hivyo kiba akamvuta mkono REHEMA na kuondoka ,
Walifika mgahawani ila siku hiyo ilikuwa mbaya kwa kiba alikuwa na mawazo kiasi kwamba hata kazi alikuwa akiharibu REHEMA aligundua alimuomba apumzike yeye atamalizia kila kitu ,

Ulifika mda wa kufunga mgahawa walifunga ila kiba alisema hata rudi atabaki mgahawani mpaka asubuhi ,kutokana na kiba kutokuwa sawa REHEMA ilibidi abaki na yeye

USIKOSE SEHEMU INAYO FUATA like Page kwa saport zaidi

MOYO WA MASIKINI 💔Sehemu ya nne🌹🌹Simulizi zetu pageNjombe Tanzania🌹AYUNI ANAMCHUKUA KIBA NA KWENDA NAE MJINIKiba alionek...
17/01/2024

MOYO WA MASIKINI 💔

Sehemu ya nne🌹🌹

Simulizi zetu page

Njombe Tanzania🌹

AYUNI ANAMCHUKUA KIBA NA KWENDA NAE MJINI

Kiba alionekana mshamba sana hakuna sehemu aliyo lala macho nje ya gari muda wote ,

WANAINGIA MJINI

Kiba aliachia meno yote nje kwa mshangao " kuzuri mjini " alisema Kiba kwa sauti kubwa AYUNI alimjibu tu kwa kifupi

" kuzuri ukiwa na pesa ukipaparikia mji ni mbaya sana huu ,magorofa haya hayana msaada wowote kwako, kuna makundi ya kila aina kuna marafiki wa kila aina ,ogopa watu wa mjii huu kuliko simba na chatu mnaoishi nao kijijini , kwa sababu adui ni vizuri ukamjua kuliko akawa rafiki yako ,siku atakayo kuzuru na uaminifu wako huijui , na pia binadamu anauwezo wa kuuwa simba na chatu ,na maanisha binadamu ndio hatari kuliko simba na chatu ,na maliza kwa kusema karibu mjini KIBASU"

Kiba alikaa kimya baada ya maneno mazito ya rafiki yake , walitembea umbali kidogoo foleni ikawa kubwa Kiba akaomba msaada afunguliwe mlango mkojo umebana , kwa sababu AYUNI alitaka amtambulishe mji unasemaje akamfungulia

Kiba akawa anatafuta sehemu akojoe kila sehemu wapo watu , alizunguka sana mwisho alipata chochoro kwa bahati mbaya alishuka na begi lake na wajanja wa mjini wakajua wakuja huyu " mgeni wa mji" anamaliza kuachia kojo watu wakampora begi ikabidi aruke nao " kosa alilofanya ni kuwafuata yeye mgeni mjini"

Alikimbiza wewe wakati huo anazidi kuwa mbali na rafiki yake mwisho wale wajanja wakamzidi kete akawakosa kimoyo moyo akasema " kweli nipo mjini😂

Kiba akasema arudi alipo toka ndio akashtuka amepotea njia ya kurud amesahau , na hana simu rafiki yake nae anashanga kiba harudi akaendelea kusubiri ,akaanza kuzunguka akimuulizia kiba kwa maelezo ,jitihada zikagonga mwamba alisema tu kimoyo moyo

" wewe mtoto wa kiume pambana mpaka nitakapo kupata"

Kijijini walipata taarifa za kupotea kwa kiba waliumia sana , na hata hivyo AYUNI alitokea kumpenda sana ADA alimwekea vishawishi mwisho aliushinda moyo wa ADA

BAADA YA MIAKA 3

kiba anaonekana akiwa na mkokoteni umebeba madumu ya maji ya kutosha , anaingia nayo kwenye mgahawa na mgahawani hapo wanampokea kwa shangwe " kiba , kiba huyo , "

KIBA ALIVYO POTEA ALIPATA MSAADA KWA JAMAA MMOJA ALIYe KUWA ANAITWA RICHARD , RICHARD HUYO ALIKUWA NA MGAHAWA WAKE AMBAO NI WA KUHONGWA NA MKE WA MTU NA RICHARD PIA ANAMDOGO WAKE WA K**E ANAITWA REHEMA ,REHEMA PIA AZIPATANI NA KIBA

Kipa ananawa mikono na kuanza kutengeneza mishkaki , muda huo huo anakuja REHEMA na kuanza kufoka bila sababu ila kiba anampotezea kwa kukaa kimya

Somo kidogoo
" katika maisha jifunze kukaa kimya sababu kimya ndio jibu la kumpa mjinga , ukimjibu kwa kuongea unampa muongozo wa kukuingia, ndio maana umepewa masikio mawili mdomo mmoja , sikia sana ongea kidogo "
Tuendelee

Wakati kelele zikiendelea ghafla linakuja gari linasimama mbele ya mgahawa anashuka richi na kuagana na mwanamke mrembo ndan ya gari , yule mwanamke anamuona kiba anampungia mkono na kumsalimu " mambo kiba" kiba

Kiba anaigoma salamu kwa kukaa kimya,mwanamke anaona haitoshi anampigia simu kiba hapokea simu,mwanamke anawasha gari na kuondoka ,

Richi anafika anaingia mgahawani na anawapa hai wateja anaingia kaunta na kuangalia mauzo anakagua mazingira anamrudia kiba nje

"Vipi kiba " kiba kinyonge anajibu safi na kuiweka mishkaki vizuri ilikuwa tayari imeiva na kumuangalia usoni rafiki yake akamuuliza

" unajipenda rafiki yangu , unampenda mdogo wako , huyu mwanamke atakufikisha pabaya huyu mwanamke bwana wake anahela atakuja kukuuwa bure rafiki yangu "

Rich alikaa kimya muda Fulani na kumjibu

"Sikuelewi rafiki au unataka ukajimilikishe wewe hapa mjini ishi kwa akili , Mimi sio wewe mtu ambaye umemsubiri demu wako miaka miwili halafu unaenda kumchukua unaambiwa ameolewa yule mwanamke sio k**a ADA chali yangu nipo nae kwa miaka , sorry k**a nimekukwaza unakera ,muda wote jambo hilo tu"

KIBA alipo sikia ADA alikuwa mpole kweli ,muda huyo huyo wanasikia kelele mgahawa wa tatu REHEMA kakiwasha haswa kila dumu la maji , kiba anafika pale rehemu kashikwa roba na lijamaa huku likimkoromea , kiba alipata hasira sana

Waliwafuata na kuwaachanisha kwa nguvu akamwambia rehema tangulia akamwambia yule jamaa

" jamaa yangu usijione unamaanguvu sana Mimi sipigani kushindana , mimi napigana kutafuta heshima na weza nikakuuwa unajua nilipotea mimi , na sitaki nikuone ukimshika rehema wetu"

Rehem anaonekana akisikiliza kwa kuibia .

USIKOSE SEHEMU INAYO FUATA

NILIKATA TAMAA. 🎸🎷🎤🎼Sehemu ya pili 🔈🔉🔊Ukurasa wa Simulizi zetu 📒📓 Njombe Tanzania 🖋📨📤🌹🌹BAADA YA MALAIKA KUSHUKA KUMBARIK...
13/01/2024

NILIKATA TAMAA. 🎸🎷🎤🎼

Sehemu ya pili 🔈🔉🔊

Ukurasa wa Simulizi zetu 📒📓

Njombe Tanzania 🖋📨📤

🌹🌹

BAADA YA MALAIKA KUSHUKA KUMBARIKI YULE MTOTO inaendelea

Malaika alimwambia yule mtoto " ishi k**a zawadi , wafariji watu wetu , utunze nyota na kipaji kwa sababu kila mtu anatamani awe k**a wewe"

Wazazi wa mtoto walimpa jina mtoto KINETIANI " faraja yetu"

Najua wewe msomaji ulitamani uwe k**a huyo mtoto , uwe mtu maalumu .

Tunaendelea .
Ilipita miezi kadhaa mtoto akiwa anakuwa kwa afya njema na uangalizi wa wazazi hao

Mtoto alikuwa wa ajabu sana hasa upande wa muziki maana hata awe na maumivu kiasi gani , ukimwimbia tu anaacha kulia

Alipo kuwa akitembea , walikuwa nae makini zaidi kwa hatari zote , walihofia zaidi mtoto kupotea alikuwa na tabia ya kufuata watu wanao imba hasa wapiga ngoma " kijijini hapo walikuwa na utaratibu wa kupiga ngoma na kuimba kila baada ya siku saba, siku za ndoa , siku za msiba , walikuwa wakizunguka kila kitongoji "

Mtoto huyo alikuwa akipenda wanavyo imba na kupiga ngoma zile

Mtoto alipo fika miaka sita ndio kipaji na nyota vikaanza kuonekana , hicho kipaji walikuwa wakijua wanafamilia tu

Mama alimkataza mwanae kuimba mbele za watu akiofia watu wenye wivu , kwa hiyo mtoto alikuwa akitaka kuimba anasubiri afike nyumbani aanze kuimba na atakaye mkuta nyumbani aliendelea hivyo hadi alipo fika miaka kumi .

BAADA YA MIAKA MINNE

MAMA " wewe mwanangu kula taratibu Leo mwalimu wenu atachelewa kuja kuwafundisha

KINE " mama mwalimu alisema nikiwahi nifanye mazoezi na wenzangu hata k**a yeye hayupo si unajua Mimi naweza kuimba kuliko watoto wote hapa kijijini "

MAMA " hahaha mwanangu na EMA mtoto wa SIKU NNE yule nae si anaweza k**a wewe"

KINE " mama , EMA anaweza ila kwangu Mimi hanifikii hata robo sababu Mimi na sauti nzuri ya kuimba kuliko yeye "

MAMA " hamna wote mpo sawa , hakuna binadamu aliye zaidi ya mwenzak kwa kila kitu ,kwa sababu sisi sote mungu wetu mmoja "

KINE " alinambia mwalimu , Mimi na kipaji cha tofauti ndio maana hata shuleni mimi ndio mwimbaji ninaye tegemewa japo kuwa kuna wanafunzi wakubwa zaidi yangu "

MAMA " kula huendage , maana unanizidi kiswahili ila uwi kurudi umpitie baba yako bustanini si unajua muda wa kumwagilia baba yako anapenda sana uwepo wewe kuliko Mimi "

KINE " EEH , alinambia kwa sababu mwanamke ni wakulinda nyumba na Mimi ni mtoto wa kiume natakiwa kujifunza kazi nikiwa mdogo "

MAMA " kaone k**a baba yake hivi "

Yalikuwa maongezi ya mama na mtoto baada ya mtoto kutoka shuleni na muda huo huo alitakiwa kwenda kanisani kufanya mazoezi ya kuimba

KINE anafika kanisani anamkuta EMA mbele akiwa bado ananguo za shule , inamaana EMA hakupitia nyumbani

KINE " wewe EMA umewahi kuliko Mimi unataka kuwa mwimbaji mzuri ?"

EMA " ndio nataka kuwa k**a wewe , mwalimu alinambia nifanye mazoezi sana "

KINE " mmh , umewahi mno , ila kwa upande wa nyie wasichana hakuna anaye kuzidi kuimba

EMA " hahaha, kweli ila Mimi njaa inaniuma , nisindikize kwenye bustani ya masista nikachume matund "

KINE " naogopa , ila twende si unanjaa "

Walienda kuiba matunda , wakiwa wanachuma walitolewa mbio na sista aliye kuwa akisafisha mazingira , yule sista alikuwa na hasira sana sababu imezoeleka kila siku matunda yanahalibiwa

Siku hiyo aliona asiwaachie watoto hao, wakina KINE walikimbia sana mwisho walifichama sehemu , sista alipo wakosa aliondoka

EMA alikuwa muoga sana KINE ALIMUULIZA

KINE " unaogopa "

EMA " ndio "alijibu huku analia

KINE " usiogope , bado unanjaa?"

EMA " ndio , "

KINE " usijali Leo tusiende kwenye mazoezi tumesha haribu yule sista atakuja kututafuta hapa twende kwenye bustani ya baba yangu , kuna matunda pia"

Wakati wanataka kuondoka EMA alishindwa kusimama kwa sababu alikuwa ameumia mguuni kwe harakati za kukimbia KINE alipiga hesabu ya haraka akaona bora ambebe tu

Wakiwa njiani walipiga stori nyingi huku EMA akiwa mgongoni mwa KINE " sababu ya EMA kuto rudi nyumbani kwao mchana huo , anaishi na mama wa kambo ambaye huwa anamzuia kwenda kuimba na kumpa kazi nyingi "

Walifika bustanini EMA akiwa hana kiatu mguu mmoja, alimshusha EMA na kumwambia atulie yeye atamtafutia matunda wakati huo baba alikuwa akiwaangalia tu .

ITAENDELEA USIKOSE SEHEMU INAYO FUATA HAPO KESHO

Ukurasa Simulizi zetu tunaitaji sapot yako kwa kucomenti na kushare

NILIKATA TAMAASehemu ya kwanzaUkurasa wa Simulizi zetu "Inaanza "Mbinguni kuna malaika wengi na malaika hao wapo katika ...
12/01/2024

NILIKATA TAMAA

Sehemu ya kwanza

Ukurasa wa Simulizi zetu

"Inaanza "
Mbinguni kuna malaika wengi na malaika hao wapo katika vitengo tofauti , kuna malaika wa kusifu ambao wapo maalumu kwa ajiri ya sifa ,kuimba , kuna kitengo cha hukumu n.k ,

Kuna siku moja malaika wa sifa alikuwa akiangalia duniani na macho yake yalikuwa yakiangalia katika kijiji kimoja kinacho itwa " maana yake tupendane ,

Wanakijiji hao walikuwa wakiishi kwa amani na upendo kutokana na sababu hiyo , mungu alimtuma malaika wa kusifu hawashushie zawadi ,

, katika kijiji hiko kuna familia moja wanaonekana wakiwa katika sherehe za mavuno ambazo huwa wanakesha wakicheza ngoma na kuimba mpaka asubuhi ,

Kuna mama mjamzito alionekana akiwa katikati ya kundi la watazamaji wakifurahi ila huyo mwanamke alionekana akiwa na furaha zaidi

Muda huo huo anaonekana mume akiwa anapepesa macho anaangalia mkewe amekaa upande gani , akamuona na akamsogelea akiwa na furaha , akamuuliza

Mume " umeona kunisubiri unachelewa "

Mke " ndio yaani hapa na furaha hadi mtoto tumboni anacheza et "

Mume " kweli , acha weee ngoja nimshike , kweli amefurahi k**a mama yake "

Mke " mmh niache bhana , nataka nisoge mbele nikaone vizuri , halafu nataka mtoto wangu awe mpiga ngoma "

Mume " hata Mimi natamani "

Yalikuwa maongezi ya mume na mkewe wakiwa wanafurahia sherehe ya mavuno , basi siku hiyo ilipita

Muda wa kujifungua yule mama ulifika na mama alipata uchungu na familia yote ilikuwa karibu

Wakati mama yupo ndani na wakunga , mume alikuwa nje akisubiri mtoto kuzaliwa

Alikuja mama Mkwe na kumtia moyo mkwe wake

" nimeota mjukuu wangu ni mvulana na atakuja kufanya makubwa hapa dunia na maanisha mtoto wako atazaliwa na nyota kubwa na kipaji cha muziki niamini maneno yangu "

Yalikuwa maneno ya bibi mtarajiwa ,

Mtoto alizaliwa akiwa na afya tele ila maajabu ya mtoto baada ya kuzaliwa na kulia tu , alikaa dakika chache na kuonesha tabasamu nzuri na kunyanyua mkono wake kwa kuonesha kuitaji kugusa kitu ,

jambo ambalo lilikuwa linaendelea ulimwengu wa kiroho , malaika alishuka kumsalimu mtoto na kumpa baraka ila alikuwa haonekani kwa macho ya binadamu wengine.

KWA LEO TUNAISHIA HAPA USIKOSE SEHEMU INAYO FUATA

Endelea kufuatilia simulizi zetu hadi mwisho na usisahau kusapoti kwa comment na kushare

NILIKATA TAMAA  " katika maisha yetu ya kila siku tunakutana na mambo mengi sana , ya kukatisha tamaa na kutia moyo pia ...
10/01/2024

NILIKATA TAMAA " katika maisha yetu ya kila siku tunakutana na mambo mengi sana , ya kukatisha tamaa na kutia moyo pia , simulizi yetu itamlenga kijana mmoja ambaye aliitwa KINETIAN jina ambalo alipewa na wazazi wake alipo zaliwa sababu ya kupewa jina hilo alizaliwa na baraka zote za kimila zao , kine alipewa zawadi kubwa ya kipaji cha muziki na nyota ya ajabu yenye kung'aa , alikuwa kupeteza kibaji na nyota akiwa bado anasoma shule ya msingi , na kipaji na nyota vikarudi baadae sana alipo kuwa amekataa tamaa ,akiwa kwenye wakati mgumu ,heshima ,umarufu , vikamrudi waliomkataa mwanzo wakaamuona dhahabu , ila kabla hajarudishiwa kuna masherti alipewa na malaika , na aliyakosea na mwisho wake ukawa mauti
.Masharti gani Alipewa ?.Kipaji na nyota nani alichukua ? Na vilirudije ?.Vipi kuhusu mahusiano ya kimapenzi ? " kuna lovestory Kali kinoma humu ndani "
Mnamengi ya kuyajua sio muda mrefu inakuja katika sauti na maandishi ..

MOYO WA MASIKINI  sehemu ya PILI simulizi zetu page njombe Tanzaniainaendelea  kibasu aliondoka kwa hasira binti akiwa k...
22/09/2021

MOYO WA MASIKINI sehemu ya PILI

simulizi zetu page njombe Tanzania

inaendelea

kibasu aliondoka kwa hasira binti akiwa kazubaa , kiba anafika nyumbani anamkuta mdogo wake yupo nje amekaa ameshika shavu ,

" mama yupo wapi?"

zaru " yupo ndani kapumzika , amechoka na harusi "

" sawa Mimi nataka nikalale nipumzike akija mtu yeyote yule mwambia sipo"

zaru " hayaa hata Dada ADA ?"

"ndio mwanbie sipo"

kiba aliingia ndani na kupumzisha hasira huku moyo wake ukiwa umejaa hasira anakumbuka maneno makali ya yule mama ,anahisi kupasuka

ASUBUHI NA MAPEMA __ kiba anagongewa mlango na mdogo wake " zaru"

" kaka kumekucha huendi shambani niandae chakula"

KIBA " siendi mama kaamka salaam "

" ndio kaenda kuchimba viazi "

KIBA " haya Leo Mimi tunashinda wote"

kiba aliamka akijinyoosha nyoosha viungo anafungua mlango wa chumba chake na kuingia sebuleni anachukua kikombe cha maji anazunguka nyuma ya nyumba , kabla ya kuanza kunawa maji anamsikia ADA anamsema mdogo wake

" wewe zaru kiburi kimeanza lini hata salamu , wala kunipa Kiti"

ZaRu " shikamoo , "

"kaka yako yupo wapi "

zaru alikaa kimya hakuwa anataka kumjibu alimuangalia K**a hajamsikia vile ADA alikasilika anataka kuondoka anakutana na mama zaru "mjane"

" umefuata nini mwanangu "

ADA "shikamoo, nilikuwa na shida na kiba "

"Zaru kaka yako yupo WAP"

ZARU " sijui mama , kaka kaenda wapi "

" sawa , na wewe ADA uje baadae saiz hayupo halafu nitakuwa na mazungumzo na we we"

ADA " sawa mama"

ADA anaondoka kiba aanatokea nyuma ya nyumba na kikombe chake mswaki mkononi , akamsalimia mama yake ,mama alikuwa anamshangaa kiba bila kujali aliingia ndani akatoka nje moja kwa kwenye mfuko aliyo beba mama yake akachukua kiasi kimoja kabla hajainuka alipigwa kofi na mama yake

".mmmmmh mama"

MAMA " pumbavu wewe unaacha kusubiri tupike wewe unatafuna vibichi ukiumwa tumbo halafu hujuii utapata minyooo"

" ngoja sasa mama najua umekasirika sio kiazi ila kuhusu ADA "

MAMA "hata ungekuwa wewe baba yako siku ile shambani ulipo kula chakula bila kumjali yeye alikuambiaje nilikuwepo ujue , alikuambia katika maisha yako usijalibu kumfanyia mtu kitu chochote ambacho wewe hupendi kufanyiwa "

" sawa , ila mama samahani siitaji kuongea Sana k**a wewe ulipenda kuzalilishwa na mama yake Sababu yeye mimi hapana "

MAMA" hallo , litoto wewe sijui nikupeleka wapi aah"

" nipeleke china nikaone magorofa makubwa marefu k**a ubongo wangu , ZARU mdogo wangu mama ananjaa mpikie ale mimi naenda kwa kina AZA "

MAMA " asubuhi Unaenda kwa watu kufanya nn k**a kuku vile"

kiba aliondoka wakati huo mama yake alikuwa akiongea pekee yake "

ADA akiwa njiani anaenda nyumbani alikumbuka aliagizwa sukari aliona bora akanunue kabisa asije akasahau wakati anavuka barabara ya gari

" barabara ambayo walichimba wananchi kwa jembe ya mkono kutokana na kuzawadio gari na mbunge kwa kuweza kulima chakula kingi ambacho kililisha wilaya nzima , mazao yalikuwa yanasafirishwa kupitia gari la zawadi pamoja na kuwasafirisha wagonjwa kwa hiyo 60% ya wanakijiji wanajua dunia nzima kuna gari moja tu ambalo walipewa zawadi "

Alikuta gari lingine ambalo ni jeusi la gharama balaa alisimama kulishngaa nalo gari likasimama

" ADA MAMBO "

ADA " AYUNI umerudi aah hallo mungu mkubwa "

" njoo hapa sasa , umekuwa mrembo mmmh npe namba ya simu"

ADA " simu !!!!!!!??????? haha hah hahaha"

" hahha na Mimi nilijua nipo mjini "

ADA " KIBA alikuwa anakusubiri "

" ndio naenda kwake kwanza kabla ya kwenda kwa Bibi yang u"

waliachana kihivyo Ila AYUNI alitokea kumpenda sana kwa ADA alivutiwa mazima ,AYUNI akutembea kitambo kirefu alimkuta kiba njiani alipiga oni kiba alishtuka kwa hasira aliokota jiwe alizani kitu gani hicho chenye matairi K**a gari LA kijiji AYUNI alifungua mlango akamwita kinyaru " kipaka " kiba alijikuta anaangalizia meno , hakuamini rafiki yake karudi toka aachane miaka 5 hivi alibeba fimbo

" acha utani kiba fimbo hiyo "

KIBA " kwanini uje bila taarifa , tungekuandalia hata mbizi "

" ndio nimekuja Ila nitakaa siku 3 Ila nitaenda mjini na wewe ukale maisha

SAMAHANI NI FUPI SABABU SINA MUDA WA KUTOSHA KUCHAPISHA ILA HAKIJA HARIBIKA KITU CHONDE NAOMBA SAPORT MNISAIDIE KuSHARE HATA KIKUNDI KIMOJA ANamgalau coment na like bila kusahau

page"

MOYO WA MASIKINI     sehemu ya kwanza  simulizi zetu page  njombe Tanzania kazi iendelee """" katika kijiji cha nanongwa...
19/09/2021

MOYO WA MASIKINI sehemu ya kwanza

simulizi zetu page

njombe Tanzania

kazi iendelee """"

katika kijiji cha nanongwa kuna tamaduni zilikuwa zikiendelea kuhusu binti kuolewa , kwamba binti akiolewa wazazi wanaheshimika kijijini hapo, hata baadhi ya mambo wanawawekea kipaumbele mfano uongozi , kusikilizwa kwenye vikao walifanya hivyo wakiamini kwamba ukiona mpaka binti ameolewa ,mzazi alikuwa makini na malezi ndio maana vijana wakamuona tabia yake,
kijiji hicho bado kilikuwa na uzamani sana ,hata mambo ya network ya simu mpaka mtembee kitambo kidogo ,ndio maana vijana walikuwa kufanya mapenzi mpaka uowe "sio kwetu kijana miaka 16 anamademu ,binti miaka 12 tayari uchochoro mambo ya kubalansia"
kubwa kuliko walikuwa walikuwa wanajiusisha zaidi na vilimo K**a nafaka ,bangi K**a kiungo cha mboga , n.k


kibasu ni kijana ambae ni yatima anaishi na mama yake ,baba yake alifariki kwa ajari ya shambani "aliangukiwa na mti alipokuwa anapumzika chini ya mti kufuata kivuli cha mti huo alilala usingizi upepo mkali ulipita na mti mizizi ilikuwa dhaifu ukaanguka na kumuuwa , ndio kumbukumbu kubwa katika familia ya marehemu KANUndi familia yenye watoto watatu wa kiume mmoja"
siku hiyo kibasu alikuwa akitoka shambani akiwa amebeba mzigo wa kuni anafika nyumbani anamkuta mama yake analia huku ameshika picha ya marehemu kanundi "mumewe" picha ambayo walipigwa zamani kibasu akiwa amebebwa na Dada yake huku wote wakiwa wameacha meno kutokana na kuishangaa camera

"mama na wewe unawaza unaumia pekee yako hata sisi tunaumia mama unavyo lia lia muda wote utakonda na mawazo ujue?"

mama aliondoka pale nje na kuingia kulilia ndani muda huo huo alikuja zarudi mdogo wake wa k**e

"njaaa inaniuma hakuna hata viazi ndani nipatie Nile"

zarubi" vipo ila alikuja Ada alikuachia na barua amesema muonane anataka kuongea na we we"

"kweli ngoja nijiandae niende , nitarudi kula "

ADA ni "binti wa mzee kabundi mzee ambae hana makuu ila mkewe mkorofi , anaongea maana huwa anabishana na wanawake kumi asipo lewa akilewa anauwezo wa kuvuruga kikao cha vijiji vitatu maana hachoki kuongea Ila kwa mumewe ni mpole k**a panya kamwagiwa maji " na Ada ni mrembo sifa zake zimetembea vijiji zaidi ya vinne mama yake huwa anatamani binti yake aolewe Ila wanakijiji wa kose pa kumtulizia

kibasu alijiandaa akanyoosha nguo zake kwa basi ya mkaa tengeneza mapanga na viboksi kwenye shati lake la kitenge akatupia tayari yupo njiani yeye huwa anajua mahali wanapo kutaniaga kila siku
, wanakutana wote wanaoneana haibu binti kambebea mkungu wa ndizi kwa jamaa na jamaa kabeba mauwa

" pole na shambani"

kiba " nzuri et ulikuja nyumbani kuniona ,kaniambia zaru"

" ndio kesho kunaharusi ya Dada yangu uje mume wangu vaa k**a Leo sawa"
kiba kwa haibu wote wakiangalia chini

hahaha hahahha hahahahahaa"

"twende tutembee tembee"

ADA " hamna ila kiba Leo imekuja barua ya tano nimekataa kwanini usiharakishe Mimi na mama hatuelewani sababu yako "

"sawa vumilia baba alinambia nisipende kufanya mambo kwa haraka bila umakini nitakuowa nitauza ng'ombe wawili mjini Ili watu washangae maana liharusi likuwa likuwa hadi raha nitakununulia ligauni sawa , maana kuna rafiki yangu amenihaidi atakuja baada ya miaka mitano na sasa bado wiki 3 "
ADA " nakupenda Sana kiba mbona kijijini hawata kunywa Majii siku hiyo hadi mama atajua kwann nilikuwa nakataa kuolewa "

waliondoka kila mtu na njia yake kiba alirudi nyumbani k**a kichaa kafurahi hadi mwisho huku amebeba mkungu wa ndizi akafika na kumuita mdogo wake

zaru njoo na kikapu fanya haraka

" hehehe amekupa dada ADA "

hizi kamuwekee mama hizi tule tumalize hizi nipikie mkae wa kesho asubuhi "

SIKU YA PILI kiba alikuwa njiani akienda kununua chumvi asubuhi hiyo alimuona ADA na wenzake wakiwa wamebeba masufuria ,na mizigo mingine imebebwa na punda , kibasu alimuangalia kwa ADA wote wakatabasamu


alifika nyumbani aliandaa nguo zake muda ulipo wadia yeye na familia yake waliongozana hadi kwenye harusi ngoma zilikuwa zikipigwa pamoja na watu kucheza kibasu alikuwa akiangalia huku na huku kumtafuta mpenzi wake akamuona akiwa anaandaa chakula

" muda wa chakula pangeni mstari chakula kipo cha kutosha watoto kaeni kwa makundi , msisukumane taratibu jamani , watoto msipigane , jamani chakula kipo"

yalikuwa maneno ya m.c wao maarufu , rafki zake kiba walikuja alimfuata kwa kibasu

" shemu anagawa wali na nyama "

kibasu " kaniambia niwe wa mwisho Chakula ni kingi balaa"

" safi sana Leo ni Leo hahaha"

kibasu " ndio maana yake tunabeba mpaka nyumbani"

mwishoni kibasu anapanga mstari anakinga chakula huku akipiga mahesabu cha kuanza kula " nyama au wali "
ghafla anashikwa masikio anavutwa anatereza na kudondoka chini anamwaga chakula anaumia goti anainua macho anamkuta mamaADA

" wewe kijana leo nimekuk**ata nimekunywa kwa ajiri yako unamalengo gani ? na mwanangu unataka kumcherewesha maisha ah?"

fikilia msomaji mama huyu ni anaongea hatari ,mkorofi akiwa hajalewa anajibizana na watu kumi akiwa amelewa anajibizana na vijiji vitatu hapo sasa kiba kabambwa peke yake mama akiwa amelewa .

watu walijaa kushangaa mama alikuwa wa moto mama yake kiba alipojaribu alijibiwa kidogo alikaa pembeni akilia alizalilishwa kweli mbele ya watu wengi kiba alibaki kainama tu pale pale Alipo hadi Giza likamkubwa

ADA alikuja kumpooza akiwa amembebea chakula kwenya Sahani

" chukua kula nimeshindwa kula kwa sababu huna amani mama yangu mzoee tuu na baba yangu alikuw mbali kidogo yote yasinge tokea "

kibasu aliinuka kwa hasira alipokea sahani na kumwaga chakula akiwa anaumia na mashambulizi ya mameno aliyokutana nayo jinsi mama yake mpendwa alivyo zalilishwa

Kiba " ujali muda wako k**a mama yako alivyo sema "

" unamaanisha nini "

kiba " saizi ni vibaya mke wa mtu mtarajiwa kuto kuwepo nyumbani "

" sikuelewi "

kiba " katika barua tano chagua moja jenga msingi ili nyumba ya maisha yako isiyumbe "

" sijakuelewa nini waongea kibasu"

" namaanisha mimi na wewe basi fanya mambo yako na Mimi kivyanguvyangu"

aliondoka kiba na ghazabu muda huo binti kabaki mdomo wazi haamini kinachosemwa

itaendelea

saport yenu muhimu sooon zitaanza kuja Simulizi katika mfumo wa sauti

SIMULIZI ZETU PAGE

KAENI MACHO FANS WANGUnipo free kwa sasa baada ya kuwa chini ya sheria muda wote niliokuwa kimya sasa tunaendea na stori...
17/09/2021

KAENI MACHO FANS WANGU
nipo free kwa sasa baada ya kuwa chini ya sheria muda wote niliokuwa kimya sasa tunaendea na stories zetu simulizi zetu drama ,love , comedy stories naanza na hiyo hapo '' saport yenu naitaji

Address

Njombe

Telephone

+255782623371

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Simulizi Zetu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share